NA:MWAJUMA ABDUL
Wanafunzi wa kike wanavyoangukia kwenye mikono ya wanaume wakware
Picha hizi zinatoa ushuhuda wa vikwazo wanavyokumbana navyo wanafunzi wa kike wakiwa njiani kwenda au kurudi shule.
Mwandishi wetu alimwona mwanafunzi huyu akizongwa na kijana huyu mkware katika eneo la makaburi ya Bahi Road mkoani Dodoma.
Japo wahusika walionekana kujuana, msichana huyu
anayesoma Shule ya Sekondari Kikuyu iliyopo Manispaa ya Dodoma, alikiri
kuwa maongezi yao yalikuwa yakielekea kubaya kiasi cha kuamua kukimbia.
Kadhia hii ilimkumba msichana huyu akiwa njiani. Anapoishi na ilipo shule kuna umbali wa karibu kilomita tano.
Vikwazo kwa watoto wa kike
Pamoja na mikakati iliyopo ya kuwasaidia watoto wa
kike kupata elimu, hali halisi katika maeneo mengi nchini inaonyesha
kuwa bado kuna vikwazo mbalimbali vinavyowazuia wasichana kupata haki
hiyo ya msingi
.
.
Kwa mfano, mara kwa mara wadau wa elimu kupitia
ripoti zao wamekuwa wakisema watoto wa kike nchini wakiwamo wanafunzi
hawako salama.
Wanafunzi hao ni waathirika wakubwa wa vitendo
mbalimbali vya unyanyasaji wa kijinsia ikiwamo kubakwa. Ukweli ni kwamba
wanafunzi wa kike hawako salama nyumbani, njiani wanapoelekea au kurudi
shule na hata shuleni kwenyewe.
CHANZO:MWANANCHI
CHANZO:MWANANCHI
0 comments:
Post a Comment