Friday, February 28, 2014

MAREKANI KULETA UMEME AFRIKA

Marekani kuleta umeme Afrika


Wabunge nchini marekani wameidhinisha mpango wa kuleta umeme kwa zaidi ya watu millioni hamsini katika jangwa la Sahara baraniAfrika na hivyo basi kutoa fursa kwa mradi huo wa serikali ya Obama kuanza kutekelezwa.
Mswada huo uliopitishwa na kamati ya maswala ya kigeni nchini humo unalenga kujenga megawati elfu ishirini barani Afrika ifikiapo mwaka 2020 na kuwafikia watu elfu hamsini ambao wanaishi bila umeme.
Mpango huo ulitangazwa na rais Obama wakati wa ziara yake barani afrika mnamo mwezi juni mwaka jana.
Mswada huo utahitajika kupitishwa na bunge la wawakilishi pamoja na lile la sineti lakini hatua hiyo ya kamati ya maswala ya kigeni ni dhihirisho tosha kwamba unuangwa mkono na pande zote za kisiasa.

 Nguzo za umeme kutoka nchini Marekani kelekea Afrika
moja ya transfoma zilizo tengenezwa kwa umbo dogo ili kupooza umeme

moja ya viongozi wa Tanzania akikagua mradi huo wa umeme kushoto ni Dr. slaa na kulia wakiwa ni mafundi mitambo mmoja kijana kutoka Afrika na mwingine marekani


Habari na,
               PETER DAUD.

0 comments:

Post a Comment