Na Mariam George
]Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na viongozi wa jumuiya za
wafanyabiashara wa kati wa Kariakoo na mikoani kuhusu mgogoro wa
matumizi ya mashine za kielektroniki za Mamlaka ya Mapato Tanzania
(TRA), jijini Dar es salaam, juzi. Wapili kulia ni Naibu Waziri wa
Fedha, Adam Malima. Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
Jumuiya ya
Wafanyabiashara Tanzania (JWT) imetangaza kusitisha mgomo wa
wafanyabiashara uliodumu kwa takriban siku tano kupinga notisi ya
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ya kuwapa siku 14 za kufunga Mashine za
Elektroniki za Kutoza Kodi (EFD).
Makamu Mwenyekiti wa jumuiya hiyo, Patrick
Masagati alisema jana kuwa mgomo huo umefutwa baada ya makubaliano baina
yao na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda huku akisema kimsingi hawapingi
matumizi ya mashine za EFD, isipokuwa mfumo mzima wa utozaji kodi
nchini.
jana kuwa mgomo huo umefutwa baada ya makubaliano
baina yao na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda huku akisema kimsingi hawapingi
matumizi ya mashine za EFD, isipokuwa mfumo mzima wa utozaji kodi
nchini.
“Waziri Mkuu, Pinda amesitisha notisi ya TRA ya
siku14 na ameahidi kuunda chombo kitakachopitia mfumo mzima wa kodi
nchini,” alidai Masagati.
Hata hivyo, hakuna taarifa yoyote rasmi
iliyotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu kuhusu mazungumzo hayo na Mwandishi
wake wa Habari, Irene Bwire hakupatikana pia kuzungumzia suala hilo.
Makamu huyo wa JWT alidai kuwa Waziri Mkuu
aliahidi kuchukua hatua stahiki kwa haraka baada ya kukutana na Waziri
wa Fedha na Uchumi, Saada Mkuya na watendaji wa TRA.
Masagati alisema katika mkutano huo ambao
ulihudhuriwa na wenyeviti wa jumuiya hiyo kutoka mikoani, pia
walimfahamisha Waziri Mkuu kuhusu mianya ya rushwa ndani ya Mamlaka ya
Bandari Tanzania (TPA) FROM mwananchi
0 comments:
Post a Comment