Na Mwajuma Abdul
Profesa Kaisi: Daktari wa kwanza kuzalisha kwa njia ya upandikizaji
NI Daktari alieonyesha moyo wa kuendelea na kazi licha ya kupata maradhi ya kiharusi yaliyomsababishia kupooza mkono na mguu.
Profesa Kaisi: Daktari wa kwanza kuzalisha kwa njia ya upandikizaji
NI Daktari alieonyesha moyo wa kuendelea na kazi licha ya kupata maradhi ya kiharusi yaliyomsababishia kupooza mkono na mguu.
Hapana shaka kuwa maelfu ya wanawake nchini
waliowahi kupata huduma zake wanamkumbuka bado kwa msaada mkubwa
aliowapa na kuwasaidia kushika mimba, kuwapa ushauri wa kitaalamu au
hata kuwazalisha.
Licha ya kustaafu, atabakia kukumbukwa kwa mengi hapa nchini, hasa kwa mchango wake kwenye sekta ya afya ya mama na mtoto.
Huyu si mwingine, bali ni Profesa Malise Kaisi,
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake na Mhadhiri Mstaafu wa Chuo Kikuu
Kishiriki cha Sayansi ya Tiba (Muhas). Nafika nyumbani kwake maeneo ya
Mikocheni jijini Dar es Salaam na ninamkuta akiwa amejipumzisha.
Anaanza kwa kunipa historia yake fupi ya kikazi.
Atoa damu kuokoa wagonjwa
Nia ya daktari yeyote duniani, ni kuokoa maisha ya mgonjwa. Hiyo ndiyo faraja ya wataalamu wa afya walio wengi.
Akiwa ni daktari ambaye anaipenda kazi yake,
Profesa Kaisi amewahi kujitolea damu kuwaokoa wagonjwa wake katika
dakika ambazo pengine walikuwa kwenye bonde la uvuli wa mauti
.
.
“Unajua wakati ule, damu ilikuwa ni tatizo kubwa.
Hakukuwa na benki ya damu kama ilivyo sasa, hivyo unapopata mgonjwa
anayehitaji damu na yupo mikononi mwako, lazima ujitoe mhanga” anasema
Anakumbuka mwaka 1970 ambapo alimpokea mgonjwa
aliyepata ajali mbaya na alihitaji damu. Ilibidi ajitolee damu yake ili
kumwokoa mgonjwa yule.
“Nikiwa Newala mwaka 1970 huo huo, mgonjwa wangu
aliyekuwa anajifungua aliishiwa damu sana na ikabidi nitoe damu yangu
haraka sana na kumuwekea na alipona,” anasema
Mara nyingine akiwa ndiyo kwanza ameripoti kwenye
kituo kipya cha kazi huko Mtwara, alifika na kumkuta mgonjwa akiwa
kwenye hali mbaya na hakuwa na mtu wa kumpa damu hivyo alikuwa
akisubiriwa kufa, yeye alitoa damu yake na mgonjwa akapona.
“Cha muhimu ni kufahamu kama una maambukizi au
la. Ukishajijua, unatakiwa utoe damu kama wewe ni daktari,” anasisitiza
Profesa Kaisi.
CHANZO:MWANANCHI
CHANZO:MWANANCHI
0 comments:
Post a Comment