Na Mwajuma Abdul
Mamia ya wanawake nchini wapo katika huduma ya kuzuia maambukizi toka kwa mama kwenda kwa mtoto.
Mamia ya wanawake nchini wapo katika huduma ya kuzuia maambukizi toka kwa mama kwenda kwa mtoto.
Ni mapema asubuhi katika kibaraza cha Hospitali ya
Wilaya ya Tanga iliyoko Ngamiani, makumi ya kinamama wajawazito
wameanza kuchukua nafasi katika benchi la kuingia katika chumba cha
ushauri nasaha na upimaji wa virusi vya Ukimwi (VVU) kabla ya kuendelea
na huduma nyingine za uzazi.
Kinamama hao ni tofauti na wengine ambao
wameishafanya kipimo hicho ambao wamefika hapo kwa ajili ya kuangalia
maendeleo ya hali zao na kadri muda unavyokwenda ndivyo idadi
inaongezeka kila mmoja akiwa ametoka umbali wake ili kuifikia huduma ya
kliniki.
Wanawake hao ni sehemu ya waelfu wengine ambao
wanakusanyika katika vituo vya huduma za afya sehemu mbalimbali nchini
kwa ajili ya huduma za kliniki ambako huko wanapimwa pia virusi vya
Ukimwi na wapo ambao wanapata huduma ya kuzuia maambukizi kutoka kwa
mama kwenda kwa mtoto.
Ripoti ya karibuni ya Wizara ya Afya na Ustawi wa
Jamii inabainisha kuwa kinamama wajawazito 69,937 waliokutwa na
maambukizi ya virusi vya Ukimwi mwaka 2012, kati yao 44,799 walipata
dawa ya kuzuia maambukizi ya mama kwenda kwa mtoto.
Idadi hiyo ni kwa wale wanawake wajawazito ambao
wameandikishwa katika kliniki za mama na mtoto na ni tofauti na wale
ambao hujifungulia nyumbani kwa wakunga wa jadi kutokana na sababu
mbalimbali ikiwa ni pamoja na umbali wa kukifikia kituo cha afya.
Ripoti hiyo inaeleza kuwa mpango huo ambao umeanza
kutekelezwa nchini toka 2011, umesaidia kupunguza maambukizi kutoka kwa
mama kwenda kwa mtoto kwa asilimia 26 mwaka 2009 hadi asilimia 15 mwaka
2012.
Kiwango hicho hata hivyo kinatajwa kuwa kidogo na
hakilingani na hali halisi na kufanya lengo la kufanya maambukizi kuwa
kufikia asilimia 4 ifikapo 2015 kwani lengo hilo huenda lisifikiwe iwapo
jitihada za maana hazitafanyika.
Ripoti hiyo ya wizara inabainisha kuwa asilimia 70
ya kinamama wajawazito nchini wapo katika tiba ya kuzuia maambukizi
kwenda kwa watoto na huduma hiyo ambayo inatolewa kwa asilimia 94 na
vituo vya afya ya uzazi.
Shirika la Umoja la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia
Watoto (Unicef), tawi la Tanzania linaeleza kuwa ni asilimia 50 pekee
ya watoto wanaozaliwa ndio wanapata huduma ya kupima virusi vya Ukimwi
na ni asilimia hiyo pia ya wajawazito wengi nchini hufika mara nne
kliniki katika kipindi cha ujauzito wao hali ambayo inafanya usimamizi
kuwa usio na mtiririko.
Pia, unyanyapaa ni sababu nyingi inayofisha mapambano dhidi ya mpango wa kuzuia maambukizi ya mama kwenda kwa mtoto.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Masula ya Afya
la Pharm Access, Geert Haverkamp anabainisha umuhimu wa huduma hiyo
katika kufikia lengo la kuhakikisha hakuna maambukizi mapyaChanzo:MWANANCHI
0 comments:
Post a Comment