NA MARYLINE OLOTU
AL AHLY imepanga kuwasili nchini leo Jumanne tayari kuikabili Yanga Jumamosi hii kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, lakini Mwanaspoti linajua kwamba matajiri wa Jangwani wamepanda mzuka na kuwatengea wachezaji wao Sh100 milioni endapo wakishinda mchezo huo.
AL AHLY imepanga kuwasili nchini leo Jumanne tayari kuikabili Yanga Jumamosi hii kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, lakini Mwanaspoti linajua kwamba matajiri wa Jangwani wamepanda mzuka na kuwatengea wachezaji wao Sh100 milioni endapo wakishinda mchezo huo.
Yanga itavaana na mabingwa watetezi hao kwenye
Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na kisha timu hizo zitarudiana wiki
mbili baadaye huko Cairo, Misri.
Yanga ikiwa na kikosi chake kamili
kitakachoongozwa na straika matata, Emmanuel Okwi, iko kambini Bagamoyo,
Pwani, ikinoa makali.
Ingawa matajiri hao walidai kwamba ahadi yao ni
siri mpaka wikiendi, habari za uhakika kutoka kwenye chanzo cha
kuaminika ndani ya benchi la ufundi, zimeeleza kuwa fedha hizo
zimeahidiwa ili kuongeza morali na kurahisisha mechi ya marudiano
ugenini.
Tayari uongozi umewapa wachezaji hao zawadi ya Sh5
milioni baada ya kuichapa Ruvu Shooting mabao 7-0 katika mechi ya Ligi
Kuu Bara hivi karibuni.
Yanga ilipanga kuwapa Al Ahly Uwanja wa Karume kwa
ajili ya mazoezi, lakini timu hiyo ikagoma na yenyewe ikaomba viwanja
vya Gymkhana na Azam Complex ambako kote wamegonga mwamba hadi
walipobahatika kwenye Uwanja wa Shule ya Kimataifa ya Tanganyika (IST).
Mechi ya Dar es Salaam itachezeshwa na Bazezew
Belete wa Ethiopia na ya marudiano itachezeshwa na Mohamed Ragab wa
Libya ambaye atasaidiwa na Fouad Fathi Farag kutoka Morocco.
0 comments:
Post a Comment