Abiria wanao
ingia na kutoka katika mkoa wa arusha wameuomba uongozi wa mkoa kuweka
utaratibu mzuri katika stendi ya mkoa ili kuepusha zoezi la abiria hao kuibiwa
mizigo yao.
Hayo
yamesemwa na baadhi ya abiria katika stendi hio, ni kutokana na msongamano wa
makondakta wanao pigia debe mabasi mbalimbali yanayo ingia na kutoka katika
stendi hio.
Kwa mujibu
wa baadhi ya makondacta wanao patikana katika stendi ya mkoa wa Arusha wamedai
kwamba tabia ya wizi katika stend hiyo inasababishwa na watu wengine haswa
wanao jifanya wabeba mizigo na matoroli sambamba na makondacta walio feki.
Na Albariki madihi
0 comments:
Post a Comment