Wednesday, September 10, 2014

ARUSHA;WANAFUNZI AJTC KUANZA MITIHANI SEPTEMBA 15 HADI 19 MWAKA HUU


Mwanafunzi Eveline Molel[Kulia], akifanya mahojiano na mwandishi wa habari wa blog hii Evelyine Bakari[kushoto]katika moja ya darasa ndani ya Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji Arusha.picha na YASINTA PETER.


Mwanafunzi Yusuph Mbata Akijisomea Kujiandaa na Mtihani,picha na YASINTA PETER

Habari na EVELYINE BAKARI                                                               
Wanafunzi wa darasa la Ruaha katika chuo cha uandishi wa habari na Utangazaji Arusha wanatarajia kufanya mitihani  ya kumaliza muhula wa kwanza kuanzia tarehe 15 mpaka tarehe 19 mwezi wa tisa mwaka huu.

Wakizungumza  na AJtc  mapema jana wanafunzi hao wamesema kuwa wamejiandaa vizuri na mitihani na wanatarajia kufaulu vizuri katika masomo yote, akizungumzia suala hilo mwanafunzi wa darasa hilo Evelyn Mollel alikuwa na haya ya kusema,

‘’Nimejiandaa vizuri na mtihani ambao tutaanza tarehe 15 mpaka tarehe 19 na ninatazamia kufaulu vizuri katika masomo yote na nina hakika  na wanafunzi wenzangu wamefanya hivyo.

Kuhusu suala la mtaala mpya wanafunzi hao wamesema ,mtaala huo ni mzuri kwa kuwa unawawezesha kujua na kupata muongozo wakati wanasoma pindi wanapokaribia kufanya mitihani kwa kuwa wanasoma mitihani waliyopewa madarasa mengine hivyo hawapati shida kufikiria wapi pa kusoma.

 Wakielezea changamoto wanazokumbana nazo kuwa ni pamoja na ukosefu wa ushirikiano kati ya wanafunzi wa darasa hilo na wengi wao kutoroka darasani kabla ya muda wa kuondoka pamoja na kubadilishiwa tarehe ya kufanya mtihani.

Pia wanafunzi hao wamemalizia kwa kuwaasa wanafunzi wenzao wa madarasa mengine  kusoma kwa bidii na waache mambo mengine na kuzingatia masomo.



0 comments:

Post a Comment