Wednesday, September 10, 2014

AFISA MAHUSIANO CHUO CHA UANDISHI WA HABARI AZUNGUMZIA MAHOSIANO BORA CHUONI


Afisa mahusiano na masoko katika chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha A.J.T.C Bw. Israeli Mungure amesema mahusiano baina ya chuo na majirani yameboreshwa kwa kuzingatia sheria na taratibu.

      Kulia:Afisa mahusiano na masoko katika chuo cha uandishi wa habari Arusha akizungumza na             mwandishi wa blogu hii Steven Mulaki.  (Picha na Winlady Johaness)

Akizungumza na mwandishi wa habari wa blogu hii bwana Mungure ameeleza njia mbalimbali ziliotumika ikiwamo njia ya kuzungumza na majirani wanaozunguka chuo hicho.
Aidha bwana Mungure amebainisha tabia waliokuwa nazo baadhi ya wanafunzi hasa wa kike ikiwa na pamoja na kuvaa mavazi yaliwakwaza majirani wa chuo hicho.

TUMEBORESHA MAHUSIANO CHUONI: Bwana Israeli Mungure kieleza kuhusu uboreshaji wa mahusiano katika chuo cha habari Arusha. (Picha na Winlady Johaness)

Hata hivyo Israeli  Mungure  ameeeleza hatua walizochukua ni pamoja na kuwaadhibu wanafunzi wanaovunja maadili hasa kwa kuvaa nguo fupi zinazowapelekea  majirani kuwa na hofu.
Vilevile bwana Mungure ameelezea uhusiano baina ya wafanyakazi  wa chuo hicho na kusema kwa sasa umeboreshwa kwa kuwa wote hufanya kazi kwa ushirikiano.
Kwa upande wao wanafunzi wa chuoni hapo wameeleza kuridhishwa na mahusiano yaliyopo baina yao na walimu pamoja na majirani wanaozunguka chuo hicho.
 Kulia:Mwanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari Arusha Theodora Massawe akizungumza na mwandishi wa blogu hii Steven Mulaki.  (Picha na Winlady Johaness)

Kadhalika mmoja wa wanafunzi bi Theodora Massawe amewaasa wanafunzi wenzie kuwa na nidhamu na kufanya yale yaliyowapeleka chuoni hapo.
Kwa upande wake Afisa Mahusiano wa chuo hicho amezitaja changamoto anazokumbana nazo katika kazi zake ikiwemo changamoto ya kuwaelewesha majirani juu ya taratibu na sheria za chuo hicho.
Aidha kwa wale majirani waliolalamikia suala la kuchota  maji bwana Mungure amewatoa wasiwasi  kwa kusema kuwa umepangwa muda maalumu wa kuteka maji chuoni hapo ikiwa ni kuanzia saa kumi jioni mpaka saa kumi na mbili jioni.
Bwana Israeli Mungure amewasihi wanafunzi kuwa makini katika masomo na kuzingatia taaluma yao inahitaji ualedi na nidhamu ya hali ya juu.


















0 comments:

Post a Comment