Thursday, March 20, 2014

Simiyu yakabiliwa na Njaa kali!!!!!!!!!!!!!




ZAIDI ya Watu lakini tano (500, 000) Mkoni Simiyu, wanakabiliwa na Njaa kutokana na kutopata Mvua, hali inayofanya Mazao yao kukauka kwa sababu ya jua.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Paschal Mabiti ametoa agizo hilo Machi 18, mwaka huu ambapo amewataka Wananchi wa Mkoa huo, wasiuze Chakula kidogo walichopata kwani hivi sasa hali ni mbaya huku akiwaagiza Viongozi wa Wilaya kuhakikisha kuwa wanadhibiti uuzwaji wa Chakula kwa baadhi ya Wananchi wa maeneo husika.

Wakielezea hali ya Chakula katika Kata zao, baadhi ya Madiwani wa Mkoa huo wamesema hali ya Chakula katika Kata zao ni mbaya kutokana na Ukame unaosababishwa na hali ya mabadiliko ya tabia ya Nchi.

Kufuatia hali hiyo Mkuu wa Mkoa amewaagiza Wananchi wa Mkoa huo, kulima Mazao yanayostahimili Ukame, kama Mtama, Viazi Vitamu na Kunde ili kuendana na Hali ya Hewa.

0 comments:

Post a Comment