Friday, March 14, 2014

Israel yaushambulia Ukanda wa Gaza

Ndege za kivita za Israel zimeyashambulia maeneo 29 ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza usiku wa kuamkia leo (13.03.2014) kujibu mashambulizi ya maroketi ya Wapalestina katika taifa hilo la kiyahudi.

Symbolbild Israel Luftangriff Gaza
Wapalestina walioshuhudia, pamoja na mpigaji picha wa shirika la habari la AFP wamesema ndege za kivita zilizishambulia kambi za watawala wa chama cha Hamas na kitengo cha kijeshi cha kundi la Islamic Jihad, Al-Quds Brigades, ambalo limedai kuhusika na mashambulizi hayo.
Taarifa ya jeshi la Israel imesema siku ya Jumatano usiku kwamba mabaki ya maroketi 60 yamepatikana, matano kati ya hayo yakisemekana kuanguka katika maeneo yenye watu wengi. Ripoti hiyo imemnukuu luteni kanali Peter Lerner akisema operesheni hiyo imefanyika kwa umakini mkubwa na bila kuchelewa. "Tumeilenga miundombinu inayowasaidia magaidi wakati wanapopata mafunzo, kupanga na kutekeleza mashambulizi yao. Hawataruhusiwa kupanga njama katika usalama wa mahekalu ya magaidi," ikaendelea kusema ripoti hiyo.
Wapiganaji wa Al-Quds Brigades wamesema wamefyetua maroketi 90 nchini Israel kulipiza kisasi mauaji ya wenzao watatu waliouwawa siku ya Jumanne kusini mwa Gaza katika shambulizi la angani la jeshi la Israel. Wapiganaji hao wametoa tamko wakisema mashambulizi yao yataendelea kujibu hujuma ya Israel ya Jumanne wiki hii. Hamas imeionya Israel dhidi ya kuchochea makabiliano.

0 comments:

Post a Comment