Tuesday, August 12, 2014

Warembo watakiwa kuwa makini na vipodozi wanavyotumia



 Aliyekaa ni Mkufunzi wa chuo cha  uandishi wa habari na utangazaji Arusha Bi.Neema Ezekiel Mwaipela akifanya mahojiano na mwandishi wa habari A.J.T.C, Irene Lyimo

Mkufunzi wa Chuo cha Uandishi  wa habari na Utangazaji Arusha  Neema Ezekieli Mwaipela  ameongea na warembo wa chuoni hapo kuhusu urembo wa kujichubua kwani  urembo huo una madhara makubwa sana  na ni hatari kwa afya zao.

Hata hivyo amewaambia  warembo hao urembo wa kujichubua siyo urembo bali ni kuharibu sura  na uhalisia wa ngozi zao, na ameendelea kuwa  elimisha kuhusu urembo huo  wapo watu wengi wanaoona kwamba mtu mweupe ni mtu mwenye hadhi kubwa ya kifedha ila sivyo wanavyofiri.

Mwaipela pia ameweza kuwapa warembo hao tofauti kati ya urembo na uzuri “ ladies urembo una maanisha ni pale ushamaliza kuoga na ukajipaka makorokoro na maanisha ukajifanyia make up, na Uzuri ni pale mtu hajajipaka chochote kajipaka tuu mafuta usoni”.

Sanjari na hayo ameelezea athari za urembo wa kujichubua kuwa zinaleta madhara makubwa sana na ni hatari kwa afya , athari hizo ni kama kuharibu maumbile yao, kupoteza ngozi zao asilia,pamoja na kupata watoto ambao hawapo vizuri kimaumbile. 

Amehitimisha kwa kuwa shauri warembo hao kuwa wabaki na uzuri “uhalisia” wao wa kuzaliwa na siyo watafute urembo ambao utakuja kuwasababishia matatizo ha[po mbeleni hata kama siyo kwa sasa.

 Na. IRENE LYMO.

0 comments:

Post a Comment