KUNDI LA PANYA LAMUUA MTOTO KWA KUMTAFUNA
HABARI NA ELIZABETH SAID
Taarifa kutoka mjini Johannesburg Afrika Kusini zinasema - kuwa panya walimng'ata mtoto wa mwezi mmoja vidole na pua .
Mtoto huyo anasubiri kufanyia upasuaji wa kuumba maumbile yake ya usoni baada ya tukio hilo huko Alexandra, JohannesburgPanya walimvamia Erena Yekanyi nyumbani kwao katika kitongoji duni cha Alexandra. Wazazi wake wanasema kuwa hawana fedha za kumpeleka hospitalini kwa matibabu anayohitaji kwa haraka baada ya kunga'twa jumatatu.
“Nilikuwa
nafua hapo nje naye Erena alikuwa ndani amelala.Mara nikamsikia akilia
ndipo nikakimbia ndani kuangalia kulikoni nilimpata anavuja damu
''alisema mamake Thandaza.
Sasa mtoto huyo anasubiri kufanyiwa upasuaji
ambao utaumba upya pua lake na pia vidole vitatu vilivyong'atwa .
Mamake anasema madaktari katika hospitali ya Charlotte Maxeke AcademicHospital wanasubiri
achangishe pesa za kutosha operesheni hiyo. Kulingana na ripoti hiyo
tukio hilo sio la kwanza katika makazi hayo duni.
Inadaiwa kuwa
watoto wengi na wazee wameripotiwa kung'atwa na panya hao wanaoonekana
sio wa kawaida kutokana na kimo chao. Msemaji wa mji wa Johannesburg
Nkosinathi Nkabinde panya ni wengi katika mitaa hiyo kutokana na hali
duni ya usafi. Amesema kuwa kuna mipango ya kuangamiza wanyama hao.
0 comments:
Post a Comment