Juzi simanzi ma majonzi vilitawala katika viwanja vya Leaders Club
wakati mamia ya watu walipokuwa wakiaga mwili wa muongozaji wa filamu na
vipindi vya televisheni, George Tyson aliyefariki katika ajali ya gari.
Moja kati ya matukio yaliyowatoa machozi mamia ya watu waliohudhuria
katika tukio la kumuaga Tyson, ni pale mtoto wake wa kike aitwae Sonia
alipokuwa akitoa neno/ujumbe wa kumuaga baba yake.
Sonia aliongea kwa majonzi maneno yaliyosababisha watu wengi watokwe machozi.
“You were kind na rafiki yangu kipenzi. Ulikuwa mtu ambaye ni
rahisi kuongea nae na kunielewa. Daima ulikuwa unanitunza na kunidekeza.
Na mara ya mwisho kuonana na wewe wiki iliyopita ulinambia ni jinsi
gani nimekufanya uwe pride na mimi. And moreover I sing…I take a breath
away. Na ninakuahidi, sitaacha kuimba kwa ajili yako. Nataka ufahamu
kwamba nitakupenda milele. I will always Love You dad. Rest In Peace.”
Sonia ni mtoto wa marehemu aliyempata na muigizaji Monalisa ambaye pia ni mtangazaji wa 100.5 Times Fm.
credit: eddy blog
Na Flaviana makawia
0 comments:
Post a Comment