Thursday, June 5, 2014

Kizimbani kwa pembe za ndovu za Sh5 bilioni


Wakili Hilla alidai vipande hivyo vilivyokuwa na uzito wa kilo 1,889, mali ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kibali cha Mkurugenzi wa Wanyamapori.
Wafanyabiashara wawili wakazi wa Dar es Salaam wamepandishwa kizimbani mbele ya Hakimu Frank Moshi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jana na kusomewa mashtaka matatu ya kufanya biashara ya pembe za ndovu zenye thamani ya zaidi ya Sh5.4 bilioni.
Washtakiwa hao, Salvius Matembo (39) na Manase Philemon (39) walisomewa mashtaka yao na Wakili wa Serikali, Pius Hilla aliyedai kati ya Januari Mosi, 2000 na Mei 2014, washtakiwa hao walisafirisha na kuuza vipande 706 vya pembe hizo.
Wakili Hilla alidai vipande hivyo vilivyokuwa na uzito wa kilo 1,889, mali ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kibali cha Mkurugenzi wa Wanyamapori. Shtaka la tatu ni la kutoroka, linamhusu mshtakiwa wa pili aliyedaiwa kutoroka chini ya ulinzi wa polisi.
Wakili huyo alisema upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na kuomba tarehe nyingine ya kutajwa.
Hakimu Moshi aliahirisha kesi hiyo hadi Juni 17, mwaka huu itakapotajwa na kuamuru washtakiwa warejeshwe mahabusu hadi tarehe hiyo.




0 comments:

Post a Comment