Thursday, November 14, 2013

MKUTANO WAKUONYESHA MAHUSIANO YA KIJAMII KATI YA MAKAMPUNI YAFANYWA NA DARASA LA TARANGIRE KATIKA CHUO CHA UANDISHI WA HABARI NA UTANGAZAJI ARUSHA!!


Katika kujifunza kwa vitendo  somo la uhusiano wa kijamii wanafunzi  wa  darasa la Tarangire katika chuo  cha uandishi  wa habari na utangazaji  Arusha  wamefanya mkutano ulioonyesha mahusiano  kati ya kampuni na jamii.

Mmoja wa wanafunzi  wa darasa hilo Bi.Mgreth  Chigogwe alisema lengo la mkutano huo ni kuongeza uzoefu kwa wanafunzi waliosoma somo hilo ili kupata uelewa mpana katika taaluma hiyo ili watakapofuzu waweze kufanya kazi kwa ufanisi .

 Hata hivyo mmoja wa wakufunzi katika chuo hicho Bi.Prisca Mnzava   amesema kuwa kufanya mazoezi kwa vitendo  ni moja ya njia  ya kumjenga mwanafunzi katika msingi imara pindi wawapo chuoni.

Naye  Bw.Elifuraha Samboto ambaye  pia ni Mkufunzi  alitoa  wito kwa wanafunzi wanaosoma somo hilo waendelee kutia mkazo katika mazoezi  ya vitendo kwani ni njia ya mafanikio katika tasnia ya habari.

FUATILIA PICHA:
Mwanafunzi Mtaita Elieth aliyesimama kwenye nafasi ya Afisa mahusianoo wa kampuni akitoa maelezo mbalimbali kuhusu bidhaa inayozalishwa na kampuni yao waliyoitambulisha kwa jina la TARANGIRE.
 Mwanafunzi Gervas Danieli aliyesimama kwenye nafasi ya Mkurugenzi wa kampuni akitoa maelezo mbalimbali kuhusu bi kampuni yake waliyoitambulisha kwa jina la TARANGIRE. 
Baadhi ya wanafunzi mbalimbali wakiwa ni waandishi wa habari walioalikwa siku hiyo.
Baadhi ya wanafunzi mbalimbali wakiwa ni waandishi wa habari walioalikwa siku hiyo.
 Mwanafunzi Frida Aizack aliyesimama kwenye nafasi ya Afisa Uzalishaji wa kampuni akitoa maelezo mbalimbali kuhusu wingi wa bidhaa inayozalishwa na kampuni ya TARANGIRE. 
 Mwanafunzi Sinyatti Simon aliyesimama kwenye nafasi ya Mkemia mkuu wa kampuni ya Tarangire akielezea aina ya madawa wanayotumia kutengenezea sabuni 
 Mwanafunzi Magreth Chigogwe aliyesimama kwenye nafasi ya Afisa masoko wa kampuni akitoa maelezo mbalimbali kuhusu bidhaa inayozalishwa na kampuni yao na wanavyopata masoko ndani na nje ya Nchi kampuni hiyo  waliitambulisha kwa jina la TARANGIRE. 
 Mwanafunzi Mtaita Elieth aliyesimama kwenye nafasi ya Afisa mahusianoo wa kampuni akitoa maelezo mbalimbali kuhusu bidhaa yao ya sabuni ya kipande inayozalishwa na kampuni yao ya TARANGIRE. 

Story by: Upendo Michael & Sia Minja
Edited by: Lightness Urassa &Vivian adson
Photo by: Juma Suleiman



0 comments:

Post a Comment