]Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na viongozi wa jumuiya za wafanyabiashara wa kati wa Kariakoo na mikoani kuhusu mgogoro wa matumizi ya mashine za kielektroniki za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), jijini Dar es salaam, juzi. Wapili kulia ni Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima. Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) imetangaza kusitisha mgomo wa wafanyabiashara uliodumu kwa takriban siku tano kupinga notisi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ya kuwapa siku 14 za kufunga Mashine za Elektroniki za Kutoza Kodi (EFD).










