NICE MEDIA WORKS

KWA WAIMBAJI WA INJILI

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Showing posts with label habari za kimataifa. Show all posts
Showing posts with label habari za kimataifa. Show all posts

Monday, September 1, 2014

Mlipuko waua a mjini Paris.

na GIFT ADISON

Jengo lililolipuliwa

Mlipuko umeharibu jengo moja la ghorofa 4 kazkazini mashariki mwa Paris na kumuua mvulana mmoja huku watu kadhaa wakiwa hawajulikani walipo.
Watano kati ya wale waliotoweka wanadaiwa kuwa watoto.
Afisa mmoja wa huduma ya zima moto katika mji huo mkuu amesema haijulikani ni nini kilichosababisha mlipuko huo.
Msemaji huyo amesema kuwa maafisa wa matibabu wamepelekwa katika eneo hilo.

Putin aelekeza shutuma Ukraine Mashariki


habari EVALIYNE BAKARI
Mwanaharakati wa demokrasi aliyetuhumiwa na wapiganaji kuwa jasusi wa serikali ya Ukraine, apigwa teke na mpita njia na kuzomewa mjini Donetsk
Rais wa Urusi, Vladimir Putin, ametoa wito kufanywe mazungumzo ya haraka kuhusu uhuru wa mashariki mwa Ukraine, kama sehemu ya mazungumzo ya kumaliza vita vya huko.
Bwana Putin amenukuliwa akisema kuwa "masilahi ya haki" ya watu wanaoishi katika jimbo hilo lazima yalindwe.
Mwandishi wa BBC anasema matamshi ya Rais Putin ni ishara kuwa Urusi inataka serikali ya Ukraine izungumze moja kwa moja na wapiganaji wanaoipendelea Urusi, kuhusu amani.
Urusi ina hamu ya kuongoza mchakato huo.
Rais Putin amesema hayo siku moja kabla ya mazungumzo kuanza mjini Minsk, Belarus ( nchi jirani na Ukraine) baina ya Ukraine, Urusi na Umoja wa Ulaya, kujadili msukosuko huo.
Na Umoja wa Ulaya na serikali ya Ukraine wameonya kuwa hali katika eneo hilo inakaribia kufika kiwango ambapo hali ya zamani haitoweza kurejeshwa tena.
Na katika tukio jengine Ukraine imekabidhi askari 10 wa miamvuli kwa Urusi, na Urusi imewarejesha wanajeshi 63 wa Ukraine.

Friday, August 29, 2014

Rubani mwanamke mkenya na mafanikio yake

Rubani wa kwanza wa kike nchini Kenya sasa amepata mafanikio zaidi kwa kufuzu kuwa rubani wa kwanza mwanamke barani Afrika kushika usukani wa ndege za kisasa aina ya Boeing 787 Dreamliner.

Imemchukuwa Rubani Irene Koki Mutungi kipindi cha zaidi ya miaka ishirini kufanikiwa kuvunja pingamizi zote zinazowazuia wanawake kuingia katika taaluma hiyo inayotawaliwa na wanaume.
Koki amefanya kazi ya urubani kwa kipindi cha miaka 20

Sunday, August 24, 2014

WAWILI WAFA KWA KWA EBOLA DRC

CHANZO BBC.  HABARI NA  GEORGE HILONGA
Picha ya Maktaba ikimwonyesha mgonjwa wa Congo mwenye umri wa miaka 43 akiwa kituo cha wagonjwa wa Ebola Septemba 29,2007
Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo imesema watu wawili wamekufa kutokana na ugonjwa wa Ebola, uliolipuka kaskazini-magharibi mwa nchi hiyo.
Hao ni wagonjwa wa kwanza wa Ebola kuripotiwa nje ya Afrika Magharibi tangu kuzuka kwa ugonjwa huo huko, ingawaje haijaeleweka wazi kama vifo vya watu hao vinahusiana na mlipuko wa Ebola katika nchi za Afrika Magharibi.
Mpaka sasa watu 1,427 wamekufa kutokana na maambukizo ya virusi vya Ebola.
Shirika la Afya Duniani, WHO limesema kasi na kiwango cha milipuko hiyo hakijawahi kutokea hapo kabla.
Watu wanaokadiriwa kufikia 2,615 Afrika Magharibi wameambukizwa ugonjwa wa Ebola tangu uzuke mwezi Machi mwaka huu.
Kirusi cha Ebola
Hakuna tiba inayojulikana kutibu ugonjwa huu lakini baadhi ya watu walioambukizwa virusi vya Ebola wamepata nafuu baada ya kupewa dawa ya Zmapp iliyo katika majaribio.
Hata hivyo dawa hiyo imeadimika kwa sasa.
Pia Jumapili, mfanyakazi wa afya wa Uingereza aliambukizwa ugonjwa wa Ebola nchini Sierra Leone na kurejeshwa Uingereza akisafirishwa na ndege ya jeshi la Uingereza, RAF.
Ni mgonjwa wa kwanza Mwingereza kuthibitishwa kuambukizwa virusi vya Ebola wakati wa mlipuko wa sasa wa ugonjwa huo.
Marekani imetuma vifaa vya tiba kusaidia kupambana na mlipuko wa Ebola nchini Liberia.
Watu kadha wamekufa katika kipindi cha mwezi uliopita baada ya kuugua homa isiyojulikana katika jimbo la Equateur katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.
Jumapili, Waziri wa Afya wa DR Congo Felix Kabange Numbi amesema watu wawili kati ya wanane waliopimwa ugonjwa Ebola wamethibitika kuambukizwa ugonjwa huo.
Ameiambia BBC kuwa eneo la karantini litawekwa katika eneo la kipenyo cha kilomita za mraba 100 katika eneo la Boende ambao wagonjwa wamegundulika.
Amesema huu ni mlipuko wa saba wa ugonjwa wa Ebola nchini DR Congo.
Virusi vya ugonjwa wa Ebola kwa mara ya kwanza viligundulika nchini humo mwaka 1976 karibu na Mto Ebola.
Bwana Numbi amesema vipimo zaidi vinafanyika.
Kituo cha wagonjwa wa Ebola nchini Sierra Leone moja ya nchi zilizoathirika kwa ugonjwa huo Afrika Magharibi
Jumamosi, bunge la Sierra Leone lilipitisha sheria mpya kuwa ni kosa la jinai kuwaficha wagonjwa wa Ebola.
Tayari watu zaidi wamekufa katika mlipuko huu wa Ebola kuliko milipuko mingine iliyowahi kutokea. Kama sheria hiyo itaidhinishwa na rais, wale wanaokamatwa kwa kuwaficha wagonjwa watakabiliwa na adhabu ya kifungo jela cha kufikia miaka miwili.
Hatua hii imekuja baada ya Ivory Coast kufunga mipaka yake ya nchi ili kuzuia kuenea kwa ugonjwa wa Ebola nchini humo.
Nchi hiyo tayari imepiga marufuku safari za ndege kwenda na kutoka Sierra Leone, Liberia na Guinea.
Gabon, Senegal, Cameroon na Afrika Kusini zimechukua hatua kama hizo.
Shirika la Afya Duniani linasema upigaji marufuku safari za ndege hakusaidii, na kinachotakiwa ni madaktari zaidi na maafisa kusaidia kuwafuatilia walioambukizwa Ebola, ikiwa ni pamoja na kuwa na maabara zaidi za kuhama.
Wiki iliyopita, madaktari wawili wa Marekani waliruhusiwa kutoka hospitalini nchini Liberia baada ya kupewa dawa ya ZMapp drug, wakati ambapo madaktari watatu wa Liberia pia wanaendelea vema.
Ugonjwa wa Ebola unaenezwa kati ya binadamu kwa kugusana moja kwa moja na majimaji ya mtu aliyeambukizwa ugonjwa huo. Ni moja kati ya magonjwa hatari kuliko yote duniani, ambapo asilimia 90 ya watu wanaoambukizwa ugonjwa wa Ebola hufariki dunia.

Saturday, August 23, 2014

MAGARI YA MSAADA YAREJEA URUSI


Malori ya misaada ya Urusi

Malori yote ya msafara wa misaada kutoka Urusi ambayo yalisafiri bila idhini hadi katika eneo linalodhibitiwa na waasi mashariki mwa Ukraine siku ya ijumaa yamerudi nchini Urusi.
Afisa mmoja wa forodha amesema kuwa malori kadhaa yalikaguliwa na kurudi nchini Urusi.
Zaidi ya malori mia mbili ya misaada yalisafiri hadi katika mji wa Luhansk siku ya ijumaa,baada ya Urusi kusema kuwa imechoka kungojea idhini kutoka kwa serikali ya Ukraine.
Urusi inasema kuwa msaada huo ulikuwa wa kibinaadamu,lakini mataifa ya Magharibi yanasema kuwa unatumiwa na Urusi kuvamia Ukraine.
Kansela wa Ujerumani Angela Merkel anatarajiwa kufanya mazungumzo mjini Kiev na rais wa Ukraine Petro Poroshenko pamoja na waziri mkuu Arseniy Yatsenyuk. CHANZO BBC........HABARI NA ELIZABETH NJAU

Wednesday, August 13, 2014

habari za kimataifa ::Liberia kutumia 'Zmapp' kutibu Ebola

WHO imeruhusu dawa ya Zmapp kutumika kuzuia kuenea kwa Ebola nchini Liberia
Jopo la wataalam wa shirika la afya duniani WHO limeamua kwamba watu wanaweza kutumia dawa ambazo hazijajaribiwa katika mwili wa binaadamu kutibu ugonjwa wa ebola,iwapo maagizo fulani yataheshimiwa ikiwemo ruhusa ya mgonjwa.

Tuesday, August 12, 2014

Liberia kupatiwa dawa ya majaribio ya Ebola

Ebola Krankenhaus Liberia

Liberia imetangaza kuwa hivi karibuni itapokea dozi za dawa za majaribio ya kutibu ugonjwa wa Ebola kutoka Marekani, ambazo itazitumia kwa madaktari wawili walioambukizwa virusi hivyo.

Serikali ya Marekani ilithibitisha kuwa iliwaunganisha maafisa wa Liberia na kampuni inayotengeneza dawa hiyo iitwayo ZMapp. Katika taarifa yake, kampuni hiyo ya Mapp Biopharmarceutical yenye makao yake jimboni California, ilisema kuwa katika kujibu maombi kutoka kwa taifa la Afrika magharibi ambalo halikutajwa, ilikuwa imeishiwa na ugavi wa dawa hiyo.

Mkuu wa polisi auawa nchini Libya


Kanali Muhammad Suwaysi aliteuliwa kama mkuu wa polisi mjini Tripoli mwaka 2012


Mkuu wa polisi katika mji mkuu wa Libya Tripoli, ameuawa na watu wasiojulikana.
Kanali Muhammad Suwaysi alipigwa risasi, alipokuwa anaondoka kwenye mkutano katika eneo la Tajoura , mtaa ulio mashariki mwa mji mkuu Tripoli.

Wenzake wawili walitekwa nyara kwa mujibu wa taarifa za wizara ya ndani.

Libya imekumbwa na vurugu zinazosemekana kusababishwa na wapiganaji wa kiisilamu, ambao walisababisha harakati za kumuondoa mamlakani Muammar Gaddafi mwaka 2011.

Maelfu ya watu wamelazimika kutoroka Tripoli.

Zaidi ya miaka mitatu baada ya kuondolewa mamlakani kwa Gadaffi, jeshi la polisi nchini Libya linasemekana kuwa dhaifu,
ikilinganishwa na wapiganaji wanaodhibiti sehemu kubwa za nchi hiyo



Wapiganaji wa kiisilamu ambao wamekuwa wakizua vurugu nchini Libya
Afisa huyo aliuawa wakati alipokuwa anatoka katika mkutano na maafisa wa mtaa wa Tajoura.
Maafisa wengine wawili waliokuwa naye, walitii masharti ya washambuliaji na kuondoka kwenye gari lao huku wakitekwa nyara.
Mamia ya watu wamefariki katika miezi ya Julai na Agosti katika kile kinachoonekana kuwa kukithiri kwa vurugu.

Habari Na.IRENE LYMO.

Tuesday, March 4, 2014

Maoni:Umoja wa ulaya wasaka njia za kuitanabahisha Urusi


Mhariri wa DW Bernd Riegert

Mshikamano Madhubuti kati ya Umoja wa Ulaya na Marekani ndio Ngao itakayomtanabahisha Rais Vladimir Putin abadilishe Msimamo wake shupavu katika Mzozo wa Ukraine 

Azuwiliwe vipi, muimla,katili, anaetaka kutetea masilahi yake bila ya kujali kupoteza hadhi yake?Masuala hayo walijiuliza mawaziri wa mambo ya nchi za nje wa Umoja wa Ulaya na siku moja kabla, hata mabalozi wa jumuia ya kujihami ya NATO mjini Brussels.Jibu la suala si rahisi,kama watu hawataki kujibwaga katika operesheni za kijeshi na kusababisha mzozo usiokadirika.Vladimir Putin ni wa enzi za zamani kwasababu angali bado anaotea yale yaliyokuwepo wakati wa vita baridi.Kwa kuingilia Crimea Putin amebainisha wazi wazi bado anang'ang'ania maeneo ya ile iliyokuwa ikijulikana kama milki ya Usovieti,.

Putin ni afisa wa zamani wa idara ya upelelezi ya Urusi KGB,ni afisa wa ngazi ya juu chamani,mtu mwenye kiu cha madaraka,na sio mwanademokrasia na wala si mtu asiyekuwa na dosari,kama alivyodai miaka kadhaa iliyopita kansela wa zamani wa Ujerumani Gerhard Schröder.Hapo mtu anaweza kulalamika lakini ukweli ni kwamba Putin anaidhibiti kikamilifu Urusi .Na ndio maana watu hawana budi isipokuwa kushirikiana nae na kupatana nae ikiwa watataka kuepusha balaa lisitokee.Hisia zinasema Umoja wa Ulaya lazma uvinjari.Busara lakini zinasema watu lazma wajaribu kuituliza Urusi,kuishirikisha na kuijumuisha katika juhudi za kidiplomasia.Na hilo hasa ndilo mawaziri wa mambo ya nchi za nje wa Umoja wa ulaya walilojaribu kulifanya walipotathmini kwanza uwezekano wa kuiwekea vikwazo na kuitolea wito Urusi ipitishe hatua za kutuliza hali ya mambo.Yatatosha? Kitatokea nini ikiwa Vladimir Putin atafuata anachokitaka mweyewe?
Malumbano au Masikilizano?
Hali hii si mpya na katika historia daima imekuwa ikijirudia:Mtawala anaivamia nchi nyengine kwasababu jamii ya walio wachache au watu wenye asili ya nchi yake eti wameomba wasaidiwe.Anaikalia sehemu ya nchi hiyo kuepusha hatari isitokee.Ilitokea hivyo hivyo mwaka 1938 Adolf Hitler alipoivamia sehemu ya Tchekoslovakia.Tusielewane vibaya,Putin hawezi kulinganishwa na Hitler.Eneo la Tchekoslovakia lenye wakaazi wenye asili ya Ujerumani,lijulikanalo kama Sudetenland,mtu hawezi kulilinganisha na Crimea.Na hali pia ni nyengine ingawa mpango unaonyesha kuwa wa aina moja.Mpango ulibainika pia mwaka 2008 pale Putin alipotuma wanajeshi kuyakalia majimbo ya Abkhasia na Ossetia nchini Georgia.Na hoja zinazotolewa hivi sasa ni zile zile eti kuwahui watu wenye asili ya Urusi huko Crimea..Kama ilivyokuwa mwaka 1938 na mwaka 2008,jumuia ya mataifa ya kidemokrasia haina jengine la kufanya ila kusubiri tu kwasababu hakuna anaetaka kuchochea hatari ya kuripuka vita kwasababu ya eneo dogo la ardhi.Na hilo rais Putin wa Urusi analitamabua fika na ndio maana ana hakika,ingawa mataifa ya kidemokrasia ya magharibi yatalalamika,na pengine vikwazo kuiwekea lakini hayatokwenda umbali wa kujibu matumizi ya nguvu kwa matumizi ya nguvu.Hali kama hiyo ilitokea pia mwaka 2008,uhusiano wa kidiplomasia ulipopooza na,mikutano kususiwa,lakini uhusiano wa kawaida pamoja na Urusi,nchi muhimu kiuchumi haujakawia .
Mshikamo Madhubuti kati ya Umoja wa ulaya na Marekani
Muhimu ni kwa Umoja wa Ulaya na Marekani kuonyesha mshikamano.Urusi ikifanikiwa kuleta mfarakano,itakayokula hasara ni Ulaya hapo.Na Umoja wa Ulaya unahitaji uungaji mkono wa Marekani kwasababu mshikamano madhubuti pekee yake ndio unaoweza kumtanabahisha Putin.

Obama ataka wachunguzi kutumwa Ukraine


Hali ya wasiwasi imekumba jimbo la Crimea.
Rais Obama ametangaza mapendekezo ambayo huenda yakatoa suluhu kwa mzozo wa Ukraine, ikiwemo kuwatuma wachunguzi wa kimataifa na kuanzishwa mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Moscow na serikali mpya mjini Kiev.
Bwana Obama amejadili swala hilo kwa njia ya simu na chanzela wa Ujerumani, Angela Merkel.
Wachunguzi hao watalenga kulinda haki za watu wa kabila la Urusi waliopo katika jimbo la Crimea; na kwa upande wake Urusi itahitajika kuwaondoa wanajeshi wake katika jimbo hilo. Pendekezo hilo huenda likajadiliwa pembezoni mwa mkutano utakaofanyika nchini Ufaransa (Jumatano) ambao utawaleta pamoja wajumbe kutoka Marekani, Urusi na kwingineko kwa ajili ya kuijadili Lebanon.
Hapo awali waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Marekani John Kerry, amelaani kile amekitaja kuwa kitendo cha uchukozi kutoka Urusi dhidi ya Ukraine. Wakati wa ziara yake mjini Kiev ambapo aliweka shada la maua kuwakumbuka waandamanaji waliouwawa mwezi uliopita, bwana Kerry ameshutumu Moscow kwa kutumia uongo na vitisho kuficha ukweli.
Mwandishi wa BBC Sarah Reinsford aliyepo mjini Kiev amesema kuwa wakati akiweka shada la maua katika maeneo walikouwawa mamia ya waandamanaji mjini humo, John Kerry alikaribishwa na umati wa watu waliokuwa wakiomba msaada wa marekani.
Na hilo ndilo lililomleta hapa; kutoa msaada wa hali na mali na pia wa kisiasa kwa serikali ya mpito ya Ukraine, na pia ahadi ya msaada wa kifedha na wa kiufundi kusaidia katika kuimarisha uchumi, amesema mwandishi wetu.
Rais Putin.
Lakini zaidi ya yote bwana Kerry ameleta ujumbe kwa Moscow.
" Nadhani ni bayana kwamba Urusi imekuwa ikifanya bidii kubuni dhana ya kuiwezesha kutekeleza uvamizi zaidi. Urusi imezungumzia raia wachache wanaozungumza kirusi ambao wamezingirwa. Ukweli ni kwamba hawajazingirwa! Ukweli ni kwamba serikali mpya ya Ukraine imewajibika ipasavyo kwa kuhimiza utulivu na kujiepusha na uchokozi," amesema Bwana Kerry.
Haukuna ushahidi, amesisitiza, kwa madai ya urusi kwamba wanajeshi wake wanalinda raia wanaozungumza lugha ya kirusi nchini Ukraine akiishutumu moscow kwa kutumia uongo na vitisho kuficha ukweli.
Katika karne ya ishirini na moja, bwana Kerry ameonya, haiwezekani kuvamia taifa jingine na kisha kuamrisha matakwa yako yatekelezwe kwa kutumia mtutu wa bunduki. Na kisha akamhimiza rais Putin kuwaondoa wanajeshi wake katika jimbo la Crimea na kushughulikia malalamishi yake kupitia njia za kisheria na amani.
Lau sivyo, ameonya, kwamba Urusi itakabiliwa na vikwazo zaidi vya kiuchumi na kisiasa.