NICE MEDIA WORKS

KWA WAIMBAJI WA INJILI

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Showing posts with label habari ya kitaifa. Show all posts
Showing posts with label habari ya kitaifa. Show all posts

Tuesday, October 7, 2014

UJASIRIAMALI NI MKOMBOZI WA MAISHA..ARUSHA

Mkurugenzi wa mafunzo katika chuo cha uandishi wa habari na utangazaji arusha bwana Joseph Mayagila Akifungua semina ya ujasiriamali iliyofanyika chuoni hapo hivi karibuni...
habbari na Yasinta Peter
Wanafunzi wa chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji Arusha wametakiwa kujishughulisha na biashara pamoja na kuwa na tabia ya kujiwekea akiba kwa ajili ya maendeleo.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa chuo hicho Bw.Joseph Mayagila  wakati akifungua semina ya ujasiriamali ambayo ilifanyika kwa siku tatu chuoni hapo kuanzia tarehe 1 mpaka tarehe 3 Octoba mwaka huu chuoni hapo.

Bw.Mayagila ameongeza kuwa wanafunzi wengi hawana tabia ya kujiwekea akiba katika fedha ambazo wanatumiwa na wazazi wao kwa ajili ya matumizi na kuwaasa wanafunzi hao wawe wanajiwekea akiba kwa maendeleo yao.

Katika semina hiyo walimu wa chuo hicho waliyoa mada mbalimbali zikiwemo za mpango wa biashara,miongozo ya mjasiriamali,namna ya kutathmini biashara pamoja na nyingine nyingi ambapo wanafunzi wote wa chuo hicho walishiriki.

Pia ili kuongeza vionjo katika semina hiyo kulikuwepo na  burudani mbalimbali ambapo wanafunzi walipewa fursa ya kuonyesha vipaji vyao mbele wanafunzi wenzao na burudani hizo ni pamoja na kuimba pamoja na vichekesho.

Nao wanafunzi wa chuo hicho wamesema kuwa wamefurahishwa na uwepo wa semina hiyo kwa sababu imewafunza mambo mbalimbali juu ya ujasiriamali ambayo hawakuwa wakiyafahamu.

Mmoja wa wanafunzi hao Bi.Edna Lucas alikuwa na haya ya kusema,
‘’Semina ni nzuri na nimeweza kujifunza mambo mengi ambayo sikuwa nayajua na kwa kupitia semina hii nimehamasika kufanya biashara’’.

Akizungumza ili kuhitimisha semina hiyo makamu mkuu wa chuo Bw.Elifuraha Samboto amewataka wanafunzi  kuwaheshimu walimu na vilevile wawe na tabia ya kjisomea.

Bw.Samboto alimaliza kwabkuwashukuru walimu na wanafunzi kwa ushiriki wao katika semina ya jasiriamali.

Wednesday, September 10, 2014

ARUSHA;WANAFUNZI WAISHIO HOSTELI AJTC WATAKIWA KUTUNZA MAZINGIRA....

 Aliyeva shati jeupe ni Waziri Emmanuel Ndenshau kiongozi wa hosteli za Loliondo katika chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha akihojiwa na mwandishi wa blog hii Gift Adison.picha na TEODORA MASSAWE.


Baadhi ya wanafunzi wa hosteli wakiwa katika eneo la kantini..picha na TEODORA MASSAWE.



Baadhi ya wanafunzi wa hosteli wakiwa wanajisomea katika eneo la hosteli..picha na TEODORA MASSAWE.


Habari na GIFT ADISON,
Wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari na utangazaji arusha wanaoishi hosteli za loliondo wameomba uongozi wa hosteli hiyo kuwapatia vifaa vya kufanya usafi kwa wakati ili kuweka mazingira safi.

Wakizungumza na waandishi wa habari mapema leo wamesema kuwa wamekuwa wakicheleweshewa vifaa vya kufanya usafi kitendo kinachowapelekea mazigira ya hosteli hiyo kotoridhisha.

Mmoja kati ya wanafunzi hao aliyejitambulisha ZIARA NYATU amesema kuwa maisha ya hosteli ni mazuri endapo mazingira yatakuwa safi ili kuwaepusha na magonjwa ya milipuko kama vile kipindupindu
   ``Maisha ya hositeli yananisaidia kuwa huru kitaaluma kwani nakuwa na muda  mwingi wa kubadilishana  mawazo na wezangu na kufanya mazoezi ya vitendo katika kituo cheti cha redio hapa chuoni ``Alisema nyatu.
                   
 Pia ameeleza changamoto wanazokabiliana nazo  kuwa ushirikiano hafifu kwa wanafunzi wengine kawa kutoshiriki katika ufanyaji usafi, tabia ya wizi, uhaba wa maji safi ya kunywa, na pia kuwapelekea baadhi ya wanafunzi kuzidi kuhama kutoka katika hosteli

``wanafunzi wengi wanatoka sehemu mbalimbali kila mtu akiwa na tabia yake hivyo inachukua mda kumbadilisha mtu kuendana na mazingira Fulani ambayo hajayazoea kama vile kufannya usafi wa jumla, na kuchoma taka pale zinapoonekana kujaa`` alisema nyatu 
  
Kwa upande wa kiongozi wa hosteli ya loliondo bwana Emmanuel Ndanshau amesema kuwa amekuwa akifanya vikao  chumba hadi chumba ili kuweza kuwashauri na kuwaonya pale wanapokwenda kinyume sheria na utaratibu wa hosteli

Bwana Ndanshau ameeleza matatizo anayokumbana nayo katika mazingira hayo ni gari la taka kuchelewa kufika kwa wakati pamoja na uhaba wa maji safi ya kunywa ingawa maji yanayopatikana ni ya kisima kwani sio bora kwa afya zao




  

ARUSHA;WANAFUNZI AJTC KUANZA MITIHANI SEPTEMBA 15 HADI 19 MWAKA HUU


Mwanafunzi Eveline Molel[Kulia], akifanya mahojiano na mwandishi wa habari wa blog hii Evelyine Bakari[kushoto]katika moja ya darasa ndani ya Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji Arusha.picha na YASINTA PETER.


Mwanafunzi Yusuph Mbata Akijisomea Kujiandaa na Mtihani,picha na YASINTA PETER

Habari na EVELYINE BAKARI                                                               
Wanafunzi wa darasa la Ruaha katika chuo cha uandishi wa habari na Utangazaji Arusha wanatarajia kufanya mitihani  ya kumaliza muhula wa kwanza kuanzia tarehe 15 mpaka tarehe 19 mwezi wa tisa mwaka huu.

Wakizungumza  na AJtc  mapema jana wanafunzi hao wamesema kuwa wamejiandaa vizuri na mitihani na wanatarajia kufaulu vizuri katika masomo yote, akizungumzia suala hilo mwanafunzi wa darasa hilo Evelyn Mollel alikuwa na haya ya kusema,

‘’Nimejiandaa vizuri na mtihani ambao tutaanza tarehe 15 mpaka tarehe 19 na ninatazamia kufaulu vizuri katika masomo yote na nina hakika  na wanafunzi wenzangu wamefanya hivyo.

Kuhusu suala la mtaala mpya wanafunzi hao wamesema ,mtaala huo ni mzuri kwa kuwa unawawezesha kujua na kupata muongozo wakati wanasoma pindi wanapokaribia kufanya mitihani kwa kuwa wanasoma mitihani waliyopewa madarasa mengine hivyo hawapati shida kufikiria wapi pa kusoma.

 Wakielezea changamoto wanazokumbana nazo kuwa ni pamoja na ukosefu wa ushirikiano kati ya wanafunzi wa darasa hilo na wengi wao kutoroka darasani kabla ya muda wa kuondoka pamoja na kubadilishiwa tarehe ya kufanya mtihani.

Pia wanafunzi hao wamemalizia kwa kuwaasa wanafunzi wenzao wa madarasa mengine  kusoma kwa bidii na waache mambo mengine na kuzingatia masomo.



Tuesday, September 9, 2014

WANAFUZI WA AJTC WAASWA KUWA NA MWITIKIO KWENYE MASHINDANO YA UTANGZAJI

Mkuu wa idara ya utangazaji katika chuo cha uandishi wa habari na utangaziji arusha bwana Onesmo Elia Mbise akifanya  maojiano na mwanishi wetu (picha na mwanaidi omary)


Mkuu wa idara ya utangazaji katika chuo cha uandishi wa habari na utangaziji arusha bwana Onesmo Elia Mbise amewaasa wanafunzi wa chuo hicho kuwa na mwitukio pindi yanapotokea katika mashindano ya utangazaji
Amesema dhumuni la mashindano hayo ni kuinua vipaji vya utangazaji  na kuimarisha wanafunzi katika uandaji wa vipindi wa radio na Tv

Thursday, August 21, 2014

ANGALIA WANAFUNZI WA AJTC WAKIWA KATIKA MAZOEZI YA VITENDO

Baadhi ya wanafunzi wa chuo cha AJTC wakisikiliza moja ya presentation zilizokwa zikitolewa na wanafunzi wenzao hii ikiwa ni sehemu ya mafunzo kwa vitendo



 Mmoja wa wanafunzi wa chuo hicho Bahati Mshana akiwasilisha mada yake mbele ya wanafunzi

 somo la  Public raations likiwa linawasilishwa kwa vitendo na baadhi ya wanafunzi chuoni hapo 

Tuesday, August 12, 2014

Wafanya biashara wa soko la kwa morombo mkoani Arusha wameimba serikali kuboresha miundo mbinu



Wafanya biashara wa soko la kwa morombo mkoani Arusha wameimba serikali kuboresha miundo mbinu ndani ya soko hilo

Misaada ya Urusi yaelekea Ukraine

Russischer Hilfskonvoi für die Ukraine 12.08.2014

Watoa misaada ya kibinaadamu, wakiwa na shehena ya misaada hiyo kutoka Urusi leo hii limeelekea nchini Ukraine. Likiwa nchini Ukraine kundi hilo litasindikizwa na wawakilishi wa asasi ya usalama na ushirikiano ya Ulaya.

Mtuhumiwa azua kihoja mahakamani Rwanda



Rwanda imekuwa ikiendedesha harakati za upatanishi na pia kuwakumbuka waliokufa katika mauaji hayo

Mshukiwa wa mauaji ya kimbari nchini Rwanda Emmanuel Mbarushimana amekataa uendeshwaji wa kesi yake na mahakama ya Kigali kwa kutoa pingamizi kwamba hana haki zilizo sawa na mwendesha mashitaka.
Mshukiwa huyo alikabidhiwa Rwanda na nchi ya Denmark mapema mwezi wa saba mwaka huu ili kujibu mashitaka ya kuhusika katika mauaji ya kimbari ya mwaka 1994.
Mushukiwa huyo Bwana Emmanuel Mbarushimana amesema kesi yake haiwezi kusikizwa hadi pale atakapopata haki zilizo sawa na mwendesha mashitaka.

Thursday, July 3, 2014

Lowassa aweka wazi utajiri wake

Waziri Mkuu wa zamani na mbunge wa Monduli, Edward Lowassa akizungumza wakati wa mahojiano na waandishi wa gazeti hili mjini Dodoma. Picha na melina makabali

  • Lowassa alisema hayo katika mahojiano maalumu yaliyofanyika ofisini kwake wiki iliyopita mjini Dodoma.
Dodoma. Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amesema madai kwamba yeye ni tajiri hayana ukweli wowote. Amesema yeye ni mfugaji na anamiliki ng’ombe zaidi ya 800 katika Jimbo la Monduli, mkoani Arusha.
Lowassa alisema hayo katika mahojiano maalumu yaliyofanyika ofisini kwake wiki iliyopita mjini Dodoma.
 “Haya madai hayana hata chembe ya ukweli hata kidogo, isipokuwa mimi nadhani wananitakia mema kwa sababu ukiona jumba zuri wanasema la Lowassa, gari nzuri la Lowassa, kitu chochote kizuri wanasema cha Lowassa,” alisema na kuongeza:
“Wamesema uongo mwingi sana, mimi nasema tu nilichopata nimepata na sina utajiri kiasi hicho,lakini si mbadhirifu wa haki zangu ninazopata kamamshahara na haki nyingine.”
Alipotakiwa kutaja mali anazomiliki, Lowassa alisema: “Mimi ni mfugaji, nina ng’ombe zaidi ya 800 jimboni kwangu Monduli.”
Lowassa ambaye pia ni mbunge wa Monduli, alisema madai kwamba anamiliki utajiri uliopindukia yalianza kabla hajajiuzulu uwaziri mkuu na ilielezwa kuwa “maduka fulani” ni yake.
Alibainisha kuwa hata kampuni ya Alphatel ambayo wanamiliki kwenye familia yake iliwahi kuhusishwa na jengo kubwa lililojengwa na mtu mmoja mwenye asili ya Kiasia wilayani Kinondoni, Dar es Salaam likiitwa Alpha.
“Ikaonekana ni jengo langu, kule Mbezi kuna rafiki yangu mmoja walienda watu wakasema hii nyumba ya Lowassa. Yule bwana alitoka na bastola akawakimbiza. Mimi sina nyumba maeneo hayo,” alisema Lowassa.na( melina makabali)