NICE MEDIA WORKS

KWA WAIMBAJI WA INJILI

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Showing posts with label KIJAMII. Show all posts
Showing posts with label KIJAMII. Show all posts

Friday, June 6, 2014

MTOTO WA MAREHEMU TYSON "SONIA" ATOA WOSIA MZITO KUHUSU KIFO CHA BABA YAKE, SIKILIZA SAUTI YAKE HAPA

Juzi  simanzi ma majonzi vilitawala katika viwanja vya Leaders Club wakati mamia ya watu walipokuwa wakiaga mwili wa muongozaji wa filamu na vipindi vya televisheni, George Tyson aliyefariki katika ajali ya gari.
 
Moja kati ya matukio yaliyowatoa machozi mamia ya watu waliohudhuria katika tukio la kumuaga Tyson, ni pale mtoto wake wa kike aitwae Sonia alipokuwa akitoa neno/ujumbe wa kumuaga baba yake.
 
Sonia aliongea kwa majonzi maneno yaliyosababisha watu wengi watokwe machozi.
 
“You were kind na rafiki yangu kipenzi. Ulikuwa mtu ambaye ni rahisi kuongea nae na kunielewa. Daima ulikuwa unanitunza na kunidekeza. Na mara ya mwisho kuonana na wewe wiki iliyopita ulinambia ni jinsi gani nimekufanya uwe pride na mimi. And moreover I sing…I take a breath away. Na ninakuahidi, sitaacha kuimba kwa ajili yako. Nataka ufahamu kwamba nitakupenda milele. I will always Love You dad. Rest In Peace.”
 
Sonia ni mtoto wa marehemu aliyempata na muigizaji Monalisa ambaye pia ni mtangazaji wa 100.5 Times Fm.
 
credit: eddy blog
Na Flaviana makawia 

Tajiri adaiwa kumng’ata, kumchoma pasi mtumishi wake kwa miaka mitatu


  Yusta Lucas akionyesha makovu yake ya mgongoni ambayo aliyapata kwa kung'atwa na kuchomwa na pasi na mwajili wake. Picha na Esther Kabakay


Dar es Salaam. Mfanyakazi wa ndani, Yusta Lucas (20) amekumbana na masahibu yanayofanana na yale ya mtoto Nasra Mvungi (4) aliyekuwa amefungiwa kwenye boksi kwa miaka karibu minne huko Morogoro. Huyu amelazwa katika Hospitali ya Mwananyamala, Dar es Salaam akiuguza majeraha yanayotokana na kuteswa na kufungiwa ndani kwa miaka mitatu.
Binti huyo, mwenyeji wa Mkoa wa Tabora, katika Kijiji cha Kampala amedai kuwa amekuwa akiteswa na kufungiwa ndani ya nyumba na tajiri yake, Amina Maige wa Mwananyamala, Kwa Manjunju katika kipindi chote hicho. Amina anashikiliwa katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay kwa tuhuma hizo na amefunguliwa jalada namba OB/RB/9967/2014.
Akisimulia masahibu yaliyompata akiwa katika Wodi Namba Tatu ya hospitali hiyo, Yusta alisema: “Nililetwa Dar es Salaam mwaka 2010 kufanya kazi za nyumbani baada ya bosi wangu (Amina) ambaye ni binamu yangu kuzungumza na mama yangu na kuniomba nije kumsaidia kazi ndogondogo.”
Alisema aliishi vizuri na mwajiri wake huyo, lakini mwaka 2012 ndipo mambo yalipoanza kubadilika akidai kuwa Amina alianza kumwadhibu kwa kumng’ata na kumchoma kwa pasi kila alipomtuhumu kutokufanya kazi zake vizuri.
“Alikuwa akinichapa na kuning’ata sehemu mbalimbali wakati mwingine usoni, pia kunichoma kwa pasi yenye moto kila aliponituhumu kutokufagia au kupiga deki vizuri.”
Hakuwahi kupelekwa hospitali
Alisema licha ya kupata vidonda kutokana na adhabu hizo, mwajiri wake huyo hakuwahi kumpeleka hospitali na pale alipoona hali ni mbaya alimnunulia dawa... “Tunaishi wawili tu baada ya kuondoka mumewe na mtoto wake kumpeleka shule ya bweni... niliugulia hadi nikapona bila mtu mwingine kufahamu.”
“Akienda kazini anafunga geti na kunikataza kufungua hata kama mtu atagonga… sokoni nilikuwa naenda siku ambazo yeye yupo tu na huwa akiniamrisha niende haraka na kurudi pasipo kuzungumza na mtu yeyote.”
Alisema mwajiri wake huyo alikuwa akituma pesa za mshahara wake kwa mama yake akisema ndiye anayepaswa kulipwa, jambo ambalo anadhani limemfanya mama yake kuhisi mwanaye yuko katika mikono salama... “Kila alipotuma alipiga simu na kunipa niongee na mama kuhakikisha kama zimefika huku akinisimamia na baada ya hapo anachukua simu.”
Ataka kurudi kwao
Binti huyo ambaye sehemu kubwa ya mwili wake ina alama za kung’atwa meno na majeraha ya kuchomwa na pasi, alisema: “Ninaomba mtu yeyote mwenye hela, nataka nikitoka hapa hospitali nirudi Tabora kwa mama. Nina shaka na maisha yangu hapa kwa huyu mama… sitaki tena kubaki Dar es Salaam kutokana na mateso ninayoyapata.

credit: mwananchi
Na Dorcas Mdemu

Wednesday, April 16, 2014

KUHUSU BOMU LA ARUSHA POLISI WATANGAZA BINGO KWA ATAKAYEFANIKISHA KUKAMATWA KWA WALIPUAJI NIGHT PARK


Jeshi la Polisi nchini limetangaza zawadi ya Sh. milioni 10 kwa atakayewezesha kukamatwa kwa  watu waliotumia mabomu kulipua  baa ya Night Park mwishoni mwa wiki iliyopita. Katika mlipuko huo, watu 17 wameripotiwa kujeruhiwa kati ya hao, waliobaki wodini kuendelea na matibabu ni nane baada ya wengine kuruhusiwa.Wanaondelea na matibabu ni  Evance Maleko, Evarist Richard, Petro James, Christian Zakaria, Pius Shayo, Antelus Ishengoma, Sudi Ramadhani na Mariam Hansi aliyeko hospitali ya Selian.Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (DCI), Isaya Mngulu, alisema uchunguzi uliofanywa na jeshi hilo umebaini kuwa bomu lililolipuliwa Aprili 13, mwaka huu, saa 1:30 asubuhi kwenye baa hiyo, ni la kutengenezwa kienyeji.Mngulu alisema wataalamu wa mabomu waligundua bomu lingine lililokuwa kwenye mkoba ulioegeshwa kwenye kiti katika baa ya Washington,  pembeni mwa baa hiyo. “Bomu hili tumeligundua baada ya tukio hili kutokea na saa sita usiku tukaligundua, lakini halijalipuka na tunalo kwa ajili ya kuchunguza tujue limetengenezwa kwa kutumia vifaa gani,” alisema.Alisema hata  bomu hilo ni la kutengenezwa kienyeji, jambo lililowafanya waelewe hata hilo lililolipuka ni la kienyeji.Mngulu alisema kutokana na kukithiri kwa matukio hayo nchini kwa sasa, ni vema wananchi na hasa wale ambao wapo maeneo ya mkusanyiko, wakachukua tahadhari za uhakika, kwani siyo vema kumwamini hata rafiki yako.“Ni vizuri ukajiridhisha alichobeba rafiki yako kwenye mkoba na ukitilia wasiwasi bora utoe taarifa polisi na siyo kukaa kimya hadi madhara yakatokea,” alisema.Alitoa rai kwa wamiliki wa kumbi za starehe, makanisani, misikitini na maeneo ya mikusanyiko kujitahidi kuweka kifaa cha CCTV ili kuwezesha kubaini wahalifu pale uuhalifu unapotokea.Alisema hadi sasa hakuna aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo na kwa kuwa wana kifaa cha CCTV kilichofungwa Night Park, wana hakika muhusika atapatikana. Alisema matukio ya milipuko ni mengi kutokea nchini kwa sasa na yanatokea maeneo mbalimbali na siyo Arusha peke yake, isipokuwa wote wanaokamatwa na milipuko hiyo kama Dar es Salaam na Tanga ni vijana wadogo ambao hawajawahi hata kupita jeshini.Kuhusu Sikukuu za Pasaka, alisema kila mkoa umepewa maelekezo kwa Kamanda wa Polisi kutumia mbinu zao zote na vifaa walivyonavyo kama farasi na mbwa ili kulinda usalama wa ibada za sikukuu hizo.