NICE MEDIA WORKS

KWA WAIMBAJI WA INJILI

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

Tuesday, August 12, 2014

Liberia kutumia 'Zmapp' kutibu Ebola

WHO imeruhusu dawa ya Zmapp kutumika kuzuia kuenea kwa Ebola nchini Liberia

Jopo la wataalam wa shirika la afya duniani WHO limeamua kwamba watu wanaweza kutumia dawa ambazo hazijajaribiwa katika mwili wa binaadamu kutibu ugonjwa wa ebola,iwapo maagizo fulani yataheshimiwa ikiwemo ruhusa ya mgonjwa.

Tangazo hilo linajiri huku shirika hilo likitangaza kuwa idadi ya watu waliofariki kutokana na ugonjwa huo imepita watu 1000 na kwamba kasisi wa uhispania aliyeondolewa nyumbani mwake baada ya kuambukizwa ugonjwa huo amefariki.

Wafanyabiashara ''utafiti dili!!''


kushoto ni Bwana Noel Taluka Akizungumza na mwanahabari.
Wafanyabiashara kote nchini  wameshauriwa   kujikita katika shughuli za kibiashara kwa kutafuta maeneo mazuri  ya kibiashara yatakayowasaidia kujipatia kipato ili kujikwamua kiuchumi badala ya kushinda vijiweni wakilaumu serikali.  


Hayo   yamesemwa    na  mmoja wa wafanyabiashara  Bwana   Noel   Taluka   ambaye   ni  muuzaji  wa  vifaa  vya  shule na muda wa matumizi ya wavuti  wakati akizungumza na wanahabari ofisi kwake Ndani  ya  chuo  cha  uandishi  wa  habari   na  utangazaji  jijini Arusha.

Bwana Taluka    amefafanua  kwamba    wafanyabiashara waliomakini ni lazima wafanye utafiti mahususi juu ya biashara wanayotaka kuifungua ili kuwafanya waendane sambamba na mahitajio ya jamii inayowazunguka.

Thursday, July 3, 2014

Ridhiwani Kikwete amudu kikaango

Mbunge wa Chalinze Mhe. Ridhwani Kikwete leo hii imekuwa ni zamu yake kushiriki kuchat Live na wananchi pamoja na wafuasi wake kupitia Kikaangoni Live ya ukurasa wa Facebook wa EATV, ambao unahusisha familia kubwa kabisa ya mashabiki.

Ridhiwani ambaye ni mtoto wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Kikwete, kupitia ukurasa wetu wa Facebook ameweza kuelezea mambo mbalimbali yanayomhusu wakati akijibu maswali ya mashabiki wake katika ulingo wa siasa na kama mtoto wa Rais.

Ridhiwani amekiri kupata maswali mengi ambayo yamekuwa changamoto kwake ambapo yamemlenga kwa namna moja au nyingine kuhusiana na ulingo wa siasa na pia hakuacha kutoa pongezi zake kwa msanii Diamond ambaye aliiwakilisha nchi alipokuwa "nominated" katika tuzo za BET zilizofanyika hivi majuzi nchini Marekani.

Zoezi hili linafanyika kila Jumatano saa 6 mpaka saa 8 mchana kupitia www.facebook.com/eatv.tv, Like ukurasa huu kama bado hujafanya hivyo ili kuwa sehemu ya familia hii kubwa, na kaa tayari kwa staa mwingine mkali kupitia Kikaangoni Live wiki ijayo.

Wavulana 19 wameaga dunia mwaka huu katika sherehe za kuwapasha tohara wavulana

Wizara ya Afya nchini Afrika Kusini inasema kuwa wavulana kumi na tisa wameaga dunia mwaka huu katika sherehe za kitamaduni za kuwapasha tohara wavulana.

Tohara hiyo ni utamaduni unaopewa heshima kubwa katika baadhi ya maeneo ya taifa hilo.

Utamaduni wa tohara ni muhimu kwa vijana hasa kwa kuwa ni njia ya vijana kuingia utu uzima, lakini baadhi hufariki wakipitia utamaduni huo na wengine hupoteza sehemu zao nyeti.
Vijana 19 wamefariki kufika sasa na wengine 50 wako hospitalini.

Wanapokea matibabu ya kukosa maji mwilini, sehemu zao za siri kuoza na majerahe mengine mabaya.

Wazee wa kijamii wasiokuwa na mafunzo ya kufanya tohara ambao huendesha vituo vya kuwapasha tohara vijana wamelaumiwa kwa vifo kama hivyo.

Katika baadhi ya visa ambavyo vimeripotiwa, vijana hutoroka na kujiunga na vijana wengine wanaokwenda katika vituo hivyo haramu bila ya idhini ya wazazi.

Serikali imewasihi wazee wa kijamii kushirikiana na watu wenye uwezo wa kitaalamu na madaktari ili kuwapasha tohara vijana na kuzuia vifo.

Mwezi jana watu 23 walikamatwa kwa vifo vya vijana waliofariki kutokana na athari za kupashwa toihara.

Na Irene V Lymo.

Tuesday, February 25, 2014

Akamatwa Muhimbili akidaiwa kufanya utabibu kinyemela

 NA MARYLINE OLOTU
Dar es Salaam. Maofisa Usalama wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), wamemkamata mtu anayedaiwa kutoa huduma kwa wagonjwa kinyume cha utaratiba na kwamba, amekuwa akiwatapeli wagonjwa wanaokwenda kupata matibabu.
Akizungumza ofisini kwake jana, Ofisa Uhusiano wa MNH, Aminieli Eligaesha alimtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Mustafa Kitano na kwamba, amekuwa akitumia majina ya Dk Nyirabu na Koba, alikamatwa wakati akimsaidia mgonjwa mmoja.
Eligeisha alisema Februari 22 mwaka huu walipata taarifa kutoka kwa Hussein Haji kuwa, kuna daktari anaitwa Koba alitaka kumtapeli Sh200,000 ili amtafutie kazi ya udereva kwenye tawi la MNH lililopo Kahama Shinyanga.
Inadaiwa Haji alipofika Muhimbili alimpigia simu daktari huyo, lakini aliambiwa kuwa wasingeweza kuonana kwa sababu alikuwa ana kikao na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, badala yake alimtaka akutane na Dk Said Kiliwanga.
“Alimwambia kazi hiyo utakuwa analipwa Sh570,000 na posho kila siku Sh90,000, pia alimwambia amtumie namba yake ya leseni,” alisema Eligaeshi.
Akisimulia jinsi alivyonusurika kutapeliwa, Haji alidai Dk Kiliwanga (ambaye hajakamatwa) alimtaka atume fedha kwenye M-Pesa ili waonane, kitendo alichokataa na kwenda kutoa taarifa kwa walinzi wa hospitali hiyo.
Namna alivyonaswa
Eligaeshi alidai maofisa usalama wa hospitali hiyo walipata taarifa za kuwapo kwa daktari aliyeonekana akiwahudumia wagonjwa na kwenda kumkamata.
Baada ya kutiwa mbaroni, inadaiwa alipekuliwa na kukutwa na kadi tatu za kliniki za wagonjwa wa Muhimbili, kitambulisho cha Peter Daniel mfanyakazi wa hoteli moja Dar es Salaam, vipimo vya kupimia ujauzito, namba nyingi za madaktari wa Muhimbili kwenye simu yake ya mkononi na Sh167,000. Wakati akiwa chini ya ulinzi, mmoja wa wagonjwa wake, aliyefahamika kwa jina la Hassan Madika alimpigia simu na kutakiwa kwenda sehemu aliyokuwa akihojiwa. Mtuhumiwa alikiri kupigiwa simu na Madika.
Inadaiwa Haji alipofika Muhimbili alimpigia simu daktari huyo, lakini aliambiwa kuwa wasingeweza kuonana kwa sababu alikuwa ana kikao na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, badala yake alimtaka akutane na Dk Said Kiliwanga.
“Alimwambia kazi hiyo utakuwa analipwa Sh570,000 na posho kila siku Sh90,000, pia alimwambia amtumie namba yake ya leseni,” alisema Eligaeshi.
Akisimulia jinsi alivyonusurika kutapeliwa, Haji alidai Dk Kiliwanga (ambaye hajakamatwa) alimtaka atume fedha kwenye M-Pesa ili waonane, kitendo alichokataa na kwenda kutoa taarifa kwa walinzi wa hospitali hiyo.
Namna alivyonaswa
Eligaeshi alidai maofisa usalama wa hospitali hiyo walipata taarifa za kuwapo kwa daktari aliyeonekana akiwahudumia wagonjwa na kwenda kumkamata.
Baada ya kutiwa mbaroni, inadaiwa alipekuliwa na kukutwa na kadi tatu za kliniki za wagonjwa wa Muhimbili, kitambulisho cha Peter Daniel mfanyakazi wa hoteli moja Dar es Salaam, vipimo vya kupimia ujauzito, namba nyingi za madaktari wa Muhimbili kwenye simu yake ya mkononi na Sh167,000. Wakati akiwa chini ya ulinzi, mmoja wa wagonjwa wake, aliyefahamika kwa jina la Hassan Madika alimpigia simu na kutakiwa kwenda sehemu aliyokuwa akihojiwa. Mtuhumiwa alikiri kupigiwa simu na Madika.