NICE MEDIA WORKS

KWA WAIMBAJI WA INJILI

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Thursday, July 3, 2014

Kova:wawili wakamata kuhusika na mauaji ya sister


na Alicia sebastian



“Majambazi hao walikamatwa kutokana na operesheni kali inayoendelea jijini hasa baada ya kifo cha sista huyo” Kamanda Kova 
na alicia  sebastian
KWA UFUPI
  • Mmoja alikuwa dereva wa bodaboda iliyokuwa imembeba jambazi aliyetoroka na fuko la fedha na mwingine alikuwa kiongozi wa tukio hilo.

Dar es Salaam. Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, imewakamata watu wanane na kati ya hao, wawili wakidaiwa kuhusika na mauaji ya Sista wa Kanisa Katoliki, Cresencia Kapuri na wengine, uporaji wa Benki ya Barclays, Tawi la Kinondoni.
Watuhumiwa hao wawili wanadaiwa kuwa, Juni 23, mwaka huu walifanya mauaji ya Sista huyo eneo la Riverside, Ubungo, Dar es Salaam na kupora kiasi cha Sh20 milioni na nyaraka mbalimbali.
Katika tukio jingine la Aprili 15, mwaka huu watuhumiwa wengine wanadaiwa kupora Sh500 milioni za benki ya Barclays.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema majambazi hao walikamatwa kutokana na operesheni kali inayoendelea jijini hasa baada ya kifo cha sista huyo.
Kamanda Kova alisema watuhumiwa waliokamatwa kuhusiana na mauaji ya mtawa huyo wa Kanisa Katoliki, mmoja alikuwa akiendesha bodaboda na alimbeba jambazi mwenzake akiwa na fuko la mamilioni ya fedha na kutoroka nalo wakati mtuhumiwa wa pili aliyekamatwa ambaye ni mfanyabiashara, ndiye aliyekuwa kiongozi katika tukio hilo.na Alicia sebastian

na romana chuwa

IBADA MAALUM: Maaskofu wawataka Ukawa kurejea bungeni



Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimpongeza Rais wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC) ambaye pia ni Askofu wa Jimbo la Iringa, Tarcisius Ngalalekumtwa kwenye Uwanja wa Kichangani Manispaa ya Iringa jana wakati wa jubilei yake ya miaka 25 ya uaskofu. Picha na Hakimu Mwafongo na romana chuwa

KWA UFUPI
  • Baraza la Maaskofu limewataka Ukawa kurejea bungeni bila masharti yoyote.
KITAIFA

IBADA MAALUM: Maaskofu wawataka Ukawa kurejea bungeni

SHARE BOOKMARKPRINTEMAILRATING
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimpongeza Rais wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC) ambaye pia ni Askofu wa Jimbo la Iringa, Tarcisius Ngalalekumtwa kwenye Uwanja wa Kichangani Manispaa ya Iringa jana wakati wa jubilei yake ya miaka 25 ya uaskofu. na romana chuwa
 
Dar na Iringa. Baraza la Maaskofu la Kanisa Katoliki Tanzania (TEC), limewataka wajumbe wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kurudi bungeni bila masharti na kuendelea na mjadala wa Katiba kwa manufaa ya taifa.
Pia, Askofu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG), Jimbo la Mashariki Kaskazini, Geoffrey Massawe amewaomba wajumbe wa Bunge la Katiba kuungana na kuwa kitu kimoja katika mchakato wa kujadili Rasimu ya Mabadiliko ya Katiba.
Kauli hizo za maaskofu hao zimekuja siku moja baada ya ile ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kusema kuwa hatima ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu utategemea Ukawa, kurejea katika Bunge Maalumu kuipitisha Katiba Mpya kwa wakati.
Askofu Massawe alitoa ombi hilo wakati wa ibada maalumu ya sherehe ya maadhimisho ya miaka 75 tangu kuanzishwa kwa kanisa hilo nchini iliyofanyika katika Kanisa la TAG Kinondoni, Dar es Salaam.
Akitoa salamu za TEC wakati wa kuadhimisha miaka 25 ya uaskofu ya Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa kwenye Uwanja wa Kichangani, Iringa, Makamu Rais wa TEC, Mhashamu Severine Niwemugizi alisema ni vyema wajumbe hao wakarudi kwenye Bunge hilo linalotarajia kuanza Agosti 5, mwaka huu.
“Ninatumia neno kuwataka na siyo kuwaomba warejee bungeni mwezi ujao. Wasipofanya hivyo au kufanya mizengwe mingine na kutupatia Katiba isiyotufaa, nitawaomba Watanzania wote tuweke uzalendo mbele na kuikataa Rasimu ya Katiba itakayoletwa pia tuwanyime uongozi katika Uchaguzi Mkuu ujao,” alisema.
Alisema wameshuhudia mambo ya aibu katika Bunge la Katiba kabla ya kupisha Bunge la Bajeti na maoni ya wananchi yaliyokusanywa kupitia tume halali yakibezwa.
Alisema tume ile iliongozwa na wazee wenye uzoefu mkubwa waliolitumikia taifa kwa muda mrefu na kutumia fedha nyingi za walipa kodi lakini yalipuuzwa jambo ambalo siyo sahihi.
“Nchi imepoteza dira, wananchi wako njiapanda hawajui kama watapata Katiba au la na ubinafsi umechukua nafasi kuliko uzalendo kwa taifa,” alisema.
Niwemugizi aliwataka Watanzania kujitokeza kwa wingi katika kuboresha Daftari la Wapigakura na kujitokeza kupiga kura kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu na ule mkuu utakaofanyika mwakani.
Akizungumza katika hafla hiyo, Waziri Mkuu, Pinda aliwataka viongozi wa dini kuliombea taifa kuwa na amani kutokana na matukio makubwa ya Uchaguzi Mkuu na Katiba yaliyopo.
Pinda alisema amesikia ujumbe uliotolewa na Askofu Niwemugizi na kuwa kiongozi makini ni yule anayekubali kukosolewa na kufanya marekebisho.

Boti isiyotumia nahodha yavumbuliwa nchini

SHARE BOOKMARKPRINTEMAILRATING
Mvumbuzi wa boti isiyotumia nahodha, Emmanuel Bukuku akitoa ufafanuzi wakati wa Maonyesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. Picha naglory kundi

Dar es Salaam. Mamlaka ya Mafunzo na Ufundi Stadi a Maonyesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere jijini hapa jana, Mvumbuzi wa mashine hiyo, Immanuel Bukuku alisema kuwa imemchukua miezi sita kufanikisha uundaji wa mashine hiyo.
Alisema uvumbuzi huo umeambatana na majaribio ambayo yamefanyika katika Pwani ya Kigamboni na yameonyesha mafanikio makubwa na ipo tayari kwa ajili ya matumizi ikiwa na kamera za kutosha kwa ajili ya uchunguzi na kupeleka taarifa.
“Uvumbuzi umekamilika na boti ipo tayari kwa ajili ya matumizi na wadau wanakaribishwa kwa ajili ya kusaidia ufanikishaji wa utengenezaji wa boti nyingine zaidi,” alisema na kuongeza kuwa boti hiyo itakuwa inaongozwa na mashine nyingine itakayo kuwa sehemu maalumu.
Bukuku ambaye ni mwalimu wa masuala ya Sayansi na Teknolojia katika Chuo cha Veta Chang’ombe alisema amevumbua boti hiyo ambayo imetengenezwa kwa kutumia vifaa rafiki na mazingira ya bahari na inatumia mfumo wa umeme jua na mashine za kuzalisha umeme.
“Ina uwezo wa kuhisi kuwapo kwa mtu au chombo kingine jirani yake na kutoa taarifa katika sehemu ambako kinaratibiwa, pia ina uwezo wa kushambulia kwa kutumia mitutu na ina uwezo mkubwa katika masuala ya ulinzi na usalama,” alisema.
Alisema pia amefanikiwa kutengeneza injini ya ndege ambayo imeonyesha mafanikio kwa kiasi kikubwa na wakati wowote inaweza kutumika na mafanikio hayo yanachangiwa kwa kiasi kikubwa na mpango wa Veta wa kuwa na Kitengo cha Masuala ya Ufundi na Ubunifu.
“Kuna mashine na teknolojia nyingi ambazo zimevumbuliwa hapa, ni dalili njema na tuna matumaini kuwa uvumbuzi zaidi unafuata kutokana na tafiti nyingi kuonyesha dalili za mafanikio,” alisema na kuongeza kuwa kitengo hicho kimepania kubadili mwelekeo mzima wa Veta kwa hivi sasa.na glory kundi

Lowassa aweka wazi utajiri wake

Waziri Mkuu wa zamani na mbunge wa Monduli, Edward Lowassa akizungumza wakati wa mahojiano na waandishi wa gazeti hili mjini Dodoma. Picha na melina makabali

  • Lowassa alisema hayo katika mahojiano maalumu yaliyofanyika ofisini kwake wiki iliyopita mjini Dodoma.
Dodoma. Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amesema madai kwamba yeye ni tajiri hayana ukweli wowote. Amesema yeye ni mfugaji na anamiliki ng’ombe zaidi ya 800 katika Jimbo la Monduli, mkoani Arusha.
Lowassa alisema hayo katika mahojiano maalumu yaliyofanyika ofisini kwake wiki iliyopita mjini Dodoma.
 “Haya madai hayana hata chembe ya ukweli hata kidogo, isipokuwa mimi nadhani wananitakia mema kwa sababu ukiona jumba zuri wanasema la Lowassa, gari nzuri la Lowassa, kitu chochote kizuri wanasema cha Lowassa,” alisema na kuongeza:
“Wamesema uongo mwingi sana, mimi nasema tu nilichopata nimepata na sina utajiri kiasi hicho,lakini si mbadhirifu wa haki zangu ninazopata kamamshahara na haki nyingine.”
Alipotakiwa kutaja mali anazomiliki, Lowassa alisema: “Mimi ni mfugaji, nina ng’ombe zaidi ya 800 jimboni kwangu Monduli.”
Lowassa ambaye pia ni mbunge wa Monduli, alisema madai kwamba anamiliki utajiri uliopindukia yalianza kabla hajajiuzulu uwaziri mkuu na ilielezwa kuwa “maduka fulani” ni yake.
Alibainisha kuwa hata kampuni ya Alphatel ambayo wanamiliki kwenye familia yake iliwahi kuhusishwa na jengo kubwa lililojengwa na mtu mmoja mwenye asili ya Kiasia wilayani Kinondoni, Dar es Salaam likiitwa Alpha.
“Ikaonekana ni jengo langu, kule Mbezi kuna rafiki yangu mmoja walienda watu wakasema hii nyumba ya Lowassa. Yule bwana alitoka na bastola akawakimbiza. Mimi sina nyumba maeneo hayo,” alisema Lowassa.na( melina makabali)


Ridhiwani Kikwete amudu kikaango

Mbunge wa Chalinze Mhe. Ridhwani Kikwete leo hii imekuwa ni zamu yake kushiriki kuchat Live na wananchi pamoja na wafuasi wake kupitia Kikaangoni Live ya ukurasa wa Facebook wa EATV, ambao unahusisha familia kubwa kabisa ya mashabiki.

Ridhiwani ambaye ni mtoto wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Kikwete, kupitia ukurasa wetu wa Facebook ameweza kuelezea mambo mbalimbali yanayomhusu wakati akijibu maswali ya mashabiki wake katika ulingo wa siasa na kama mtoto wa Rais.

Ridhiwani amekiri kupata maswali mengi ambayo yamekuwa changamoto kwake ambapo yamemlenga kwa namna moja au nyingine kuhusiana na ulingo wa siasa na pia hakuacha kutoa pongezi zake kwa msanii Diamond ambaye aliiwakilisha nchi alipokuwa "nominated" katika tuzo za BET zilizofanyika hivi majuzi nchini Marekani.

Zoezi hili linafanyika kila Jumatano saa 6 mpaka saa 8 mchana kupitia www.facebook.com/eatv.tv, Like ukurasa huu kama bado hujafanya hivyo ili kuwa sehemu ya familia hii kubwa, na kaa tayari kwa staa mwingine mkali kupitia Kikaangoni Live wiki ijayo.

Wavulana 19 wameaga dunia mwaka huu katika sherehe za kuwapasha tohara wavulana

Wizara ya Afya nchini Afrika Kusini inasema kuwa wavulana kumi na tisa wameaga dunia mwaka huu katika sherehe za kitamaduni za kuwapasha tohara wavulana.

Tohara hiyo ni utamaduni unaopewa heshima kubwa katika baadhi ya maeneo ya taifa hilo.

Utamaduni wa tohara ni muhimu kwa vijana hasa kwa kuwa ni njia ya vijana kuingia utu uzima, lakini baadhi hufariki wakipitia utamaduni huo na wengine hupoteza sehemu zao nyeti.
Vijana 19 wamefariki kufika sasa na wengine 50 wako hospitalini.

Wanapokea matibabu ya kukosa maji mwilini, sehemu zao za siri kuoza na majerahe mengine mabaya.

Wazee wa kijamii wasiokuwa na mafunzo ya kufanya tohara ambao huendesha vituo vya kuwapasha tohara vijana wamelaumiwa kwa vifo kama hivyo.

Katika baadhi ya visa ambavyo vimeripotiwa, vijana hutoroka na kujiunga na vijana wengine wanaokwenda katika vituo hivyo haramu bila ya idhini ya wazazi.

Serikali imewasihi wazee wa kijamii kushirikiana na watu wenye uwezo wa kitaalamu na madaktari ili kuwapasha tohara vijana na kuzuia vifo.

Mwezi jana watu 23 walikamatwa kwa vifo vya vijana waliofariki kutokana na athari za kupashwa toihara.

Na Irene V Lymo.

Wednesday, July 2, 2014

BONANZA LA WANAHABARI ARUSHA LAFANA. PINTO AAHIDI KUSAIDIA KUBORESHA LIJALO

NA: NURU PAULO FERUZ

Arusha.Timu ya soka na ya mpira wa pete za Chuo Cha Uandishi wa Habari Arusha (AJTC) juzi zilitwaa ubingwa katika bonanza la tisa la waandishi wa habari Kanda ya Kaskazini.
Katika bonanza hilo, lilifanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid kwa kuandaliwa na Taswa Arusha na kampuni ya Ms Unique, jumla ya timu 10 zilishiriki kutoka mkoa wa Arusha na Manyara.
Timu ya soka ya AJTC ilitwaa ubingwa baada ya kuifunga kwa mikwaju ya penati 5-4 timu ya Radio Sunrise, wakati wasichana wa timu hiyo, waliwashinda timu ya chuo cha  uandishi wa habari na maendeleo ya jamii (IMS), magoli 18-5.
Mgeni rasmi katika bonanza Mwenyekiti wa Taswa Taifa, Juma Pinto alikabidhi vikombe na fedha taslimu, ambapo bingwa wa very soka alipewa kikombe, ,fedha taslimu 200,000 na seti ya jezi.
Huku mshindi wa pili soka akipata 100, 000 wakati bingwa wa mpira wa pete alizawadiwa kikombe cha fedha taslimu 100, 000 huku mshindi wa pili akikabidhiwa tsh 50, 000.
Katika bonanza hilo, ambalo lilidhaminiwa na kampuni ya bia nchini, (Tbl), kampuni ya Megatrade Investment, Mamlaka ya hifadhi Ngorongoro, Cocacola, SBC (T) ltd, AICC, Tanzanite Forever, TANAPA na Alphatel timu nyingine zilizoshiriki ni Radio 5.
Nyingine ni timu ya Arusha One, ORS kutoka mkoa wa Manyara, Salam Club, IMS na  Taswa Arusha Arusha ambayo iliambulia ushindi katika kukamata kuku.
Akizungumza katika bonanza hilo, Pinto alipongeza washindi na viongozi wa Taswa Arusha kwa kazi the nzuri waliofanya.
Pinto pia aliahidi katika maadhimidho ya miaka 10 ya bonanza hilo, mkutano mkuu wa T aswa Taifa utafanyik a Arusha sambamba na tuzo za waandishi bora.
Awali Meneja matukio wa TBl, Chris Sarakana aliahidi Tbl kuendelea kudhamini bonanza hilo kutokana na kuvutia wanahabari na wakazi wengi wa Arusha.
Meneja masoko wa Mega trade, Godluck Kway aliwapongeza wanahabari kwa kushiriki kwa wingi katika bonanza hilo na kuahidi kue kudhamini.

Tuesday, July 1, 2014

Je Urembo wa kujichubua ni urembo?


Picha za hivi karibuni za Vera Sidika kwenye mitandao ya kijamii
Swala la kubadili rangi ya ngozi limekuwa kama msumari moto, kunao wanaoliunga mkono na wale wanaolipinga swala hilo katu hawawezi kulifanya.

Baadhi wanasema kuwa ni wanawake wasiojithamini na kujiamini pekee ndio wenye kujichubua ngozi.

Mjadala huo ukiendelea, wasichana wengi wanajitafutia umaarufu sio Marekani na Uingereza tu bali hata katika kanda ya Afrika ya Mashariki. Wasichana hao wamekuwa wakifanya kila wawezalo ili kupata huo umaarufu.

Picha za awali kabla ya Vera kujichubua ngozi
Mmoja wa wasichana hao ni Vera Sidika anayejulikana sana nchini Kenya na Afrika mashariki kwa kuwa na makalio makubwa ambayo ndiyo yaliyompa umaarufu wake baada ya kuonekana katika wimbo mmoja wa video uitwao 'You Guy' ambao baadaye ulipigwa marufuku nchini Kenya.

Vera amejizidishia umaarufu kwa kubadili rangi yake ya ngozi, zamani kidogo akiwa mweusi na sasa amejichubua na kuwa mweupe na pia kuwaambia watu kuwa kubadili rangi ya ngozi yake ni yeye mwenyewe kujitakia. Hiyo isiwashughulishe watu.

Vera anajulikana kwa kuwa na mazoea ya kujipiga picha hasa za makalio yake na kuziweka kwenye mitandao ya kijamii. Vara analinganishwa sana na Kim Kardhashian hasa kwa sababu ya umbo lake.

Kazi ya Vera hasa ni ya uwanamitido lakini mbali na hilo Vera hulipwa ili kufika kwenye karamu mbali mbali , kwenye disco na katika hafla mbali mbali za watu mashuhuri. Yeye pia hulipwa kuwa katika kanda za video za wanamuziki maarufu Afrika Mashariki.

Alifichua kupitia televisheni Ijumaa kuwa alitumia maelfu ya dola kubadili rangi ya ngozi yake na kujifanya mweupe.

Shughuli hiyo aliifanyia nchini Uingereza na ilimgharimu karibu milioni 15 pesa za Kenya, hizo ni dola 170,000 na kwamba tayari kuna watu wengi wanaotaka sana kujichubua ngozi na kufanana na Vera, kwa mujibu wa mwanadada huyo.

Vera ni mwanamitindo na anapanga kufungua duka la kuuzwa bidhaa za urembo
Vera anasema kuwa watu wamemsema sana kwenye mitandao ya kijamii vibaya kwa sababu ya anavyoendesha maisha yake.
Amewataja kama wanafiki kwa sababu anasema huku wakiendelea kumsema na kumkosoa kwa kujichubua, wamekuwa wakimuuliza alichofanya ili na wao watafute pesa wakafanye hivyo kwa wanataka sana kufanan naye.

Mtindo wa wanawake kujichubua ni swala tata nchini Kenya. Sio kama India ambako vipodozi vya kujichubua huuzwa wazi wazi. Nchini Kenya bidhaa hizo, huuzwa kimagendo.

Wataalamu wanasema, wanawake wengi wanaendelea kujichubua licha ya hatari za bidhaa zinazouzwa kimagendo.

Swala la wanawake kijichubua barani Afrika lilianza kujadiliwa waziwazi pale ambapo msanii raia wa Cameroon Dencia kuzindua rasmi bidhaa zake za kuchubua ngozi ziitwazo, Whitenicious.

AJTC WAIBUKA KIDEDEA KWENYE BONANZA LA WAANDISHI WA HABARI MKOANI ARUSHA

Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa habari za michezo nchini(Taswa)Juma Pinto(kushoto) akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa kudumu wa Taswa mkoa wa Arusha,Jamila Omary aka "Dangote" wakati wa Bonanza la vyombo vya lililopigwa kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Mgeni Rasmi katika Bonanza la Vyombo vya Habari mkoani Arusha,Juma Pinto wa pili kushoto,akifatilia michezo iliyokua inaendelea kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha wengine kushoto ni Le Mutuz,Mkurugenzi wa Gogobichi Media,Joseph Lyimo na Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Mega Trade,Goodluck Kway

Washindi wa kukimbiza Kuku  kutoka The Institute of Media and Social Studies(IMS) "wakishow"

Katibu wa Kudumu wa Taswa Arusha,Mussa Juma(shoto) akiwa Le Mutuz baada ya kukagua timu za Arusha One Radio na Arusha Journalism Training College(AJTC)

Mabingwa katika mpira wa miguu na mpira wa Pete(Netball)Chuo cha Arusha Journalism Training College(AJTC)wakishangilia ushindi wao.

Waandishi wa habari za michezo wakifatilia burudani.

WAKUFUNZI wa Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji Arusha wakifuatilia mwenendo wa Mchezo kati ya Sunrise Redio na  Chuo cha  hicho cha AJTC

 
Baathi ya wanafunzi wa Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji Arusha wakifuatilia kwa makini Mpambano.


Katibu Msaidizi wa Taswa Arusha na Mtangazaji Mahiri wa vipindi vya Michezo na Burudani,Hamza Kalemera akichapa kazi,kulia ni Mussa Juma