Mkurugenzi wa redio faraja Bw.Simeo Makoba akisisitiza jambo kwa Waandishi wa Habari na Utangazaji. |
Mkurugenzi
wa kituo cha redio faraja Bw.Simeo Makoba amewataka waandishi wa habari kujenga
mazoea ya kujisomea vitabu pamoja na kusikiliza vyombo mbalimbali vya habari
ili kujua taarifa zinazoendelea hapa nchini na nje ya nchi.
Bwana Makoba
aliyasema hayo Mkoani Arusha alipokuwa akizungu mza na waandishi wa habari
katika Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji Arusha (AJTC) kwalengo
lakuwaimarisha kinadharia.
Akitoa ufafanuzi
juu ya taaluma ya habari Bw.Makoba amesema nivema wanahabari kujitambua ikiwa
ni pamoja na kuweka jitihada katika masomo yao kwa nadharia na vitendo.
Bw.Makoba
alisema”Waandishi wa habari ni watu wanaotakiwa kuwa wadadisi,wafuatiliaji wa
mambo pamoja na kuyafichua yale yote yanayolenga kuikandamiza jamii pamoja na
unyanyasaji”alisema Bw.Makoba
Aliendelea
kusema kuwa Ufanisi wa kazi katika tasnia ya habari umekuwa na changamoto
nyingi ambazo zipo baadhi yake zinazosababishwa
na waandishi wenyewe na pia zipo zinazochangiwa na serikali.
Amezitaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na
kutodhaminiwa, kutokupata maslahi yakutosha, vitisho vya kipigo, kutokuwa na
ulinzi pamoja na uwezeshwaji kwa wanahabari.
Hatahivyo
ametoa wito kwa wanahabari kuwa na muonekano mzuri kwa jamii pamoja na kuvaa
mavazi yanayosadifu kazi yao, pamoja na kufanya kazi ipasavyo ili kuijenga
taaluma ya uandishi wa habari.
By Virginia Daniel & Emmanuel Ndanshau.
0 comments:
Post a Comment