Wednesday, October 22, 2014
CHADEMA KUIPELEKA MAHAKAMANI KATIBA ILIYOPENDEKEZWA ISIPIGIWE KURA NA WANANCHI
2:46 AM
No comments
Chama cha Demokrasia na maendeleo
Chadema kimesema kinakamilisha ushahidi ili kwenda mahakamani kupinga
katiba inayopendekezwa kupelekwa katika hatua ya kupigiwa kura ya maoni
kwa madai kuwa katiba hiyo imekosa uhalali kutokana na kukosa theluthi
mbili kutoka upande wa Zanzibar.
Makamu mwenyekiti wa Chadema Tanzania Bara Profesa Abdalah Safari
ametoa tamkoa hilo wakati akihutubia umati wa wakazi wa mji wa Iringa na
vitongoji vyake kwenye uwanja wa Mlandege ambapo amebainisha kuwa zoezi
la kupitisha rasimu ya katiba inayopendekezwa ndani ya Bunge maalumu la
katiba liligubikwa na mbinu chafu za uchakachuaji wa kura hasa za
wajumbe wa Zanzibar.
Kwa upande wake katibu mkuu wa chama hicho Dokta Wilbrod Slaa
amesema chama cha mapinduzi kimeanza kuhujumu mchakato wa uandikishaji
wa wananchi kwenye Daftarai la Makazi kwa kuendesha zoezi hilo kwa siri
huku kikitumia mabalozi wa nyumba kumi wa chama hicho kinyume na
utaratibu wa kawaida ambapo kazi hiyo inapaswa kufanywa na watendaji wa
vijiji kata na mitaa.
Tuesday, October 7, 2014
UJASIRIAMALI NI MKOMBOZI WA MAISHA..ARUSHA
Mkurugenzi wa mafunzo katika chuo cha uandishi wa habari na utangazaji arusha bwana Joseph Mayagila Akifungua semina ya ujasiriamali iliyofanyika chuoni hapo hivi karibuni...
Hayo yamesemwa na Mkuu wa chuo hicho Bw.Joseph Mayagila wakati akifungua semina ya ujasiriamali ambayo ilifanyika kwa siku tatu chuoni hapo kuanzia tarehe 1 mpaka tarehe 3 Octoba mwaka huu chuoni hapo.
Bw.Mayagila ameongeza kuwa wanafunzi wengi hawana tabia ya kujiwekea akiba katika fedha ambazo wanatumiwa na wazazi wao kwa ajili ya matumizi na kuwaasa wanafunzi hao wawe wanajiwekea akiba kwa maendeleo yao.
Katika semina hiyo walimu wa chuo hicho waliyoa mada mbalimbali zikiwemo za mpango wa biashara,miongozo ya mjasiriamali,namna ya kutathmini biashara pamoja na nyingine nyingi ambapo wanafunzi wote wa chuo hicho walishiriki.
Pia ili kuongeza vionjo katika semina hiyo kulikuwepo na burudani mbalimbali ambapo wanafunzi walipewa fursa ya kuonyesha vipaji vyao mbele wanafunzi wenzao na burudani hizo ni pamoja na kuimba pamoja na vichekesho.
Nao wanafunzi wa chuo hicho wamesema kuwa wamefurahishwa na uwepo wa semina hiyo kwa sababu imewafunza mambo mbalimbali juu ya ujasiriamali ambayo hawakuwa wakiyafahamu.
Akizungumza ili kuhitimisha semina hiyo makamu mkuu wa chuo Bw.Elifuraha Samboto amewataka wanafunzi kuwaheshimu walimu na vilevile wawe na tabia ya kjisomea.
Bw.Samboto alimaliza kwabkuwashukuru walimu na wanafunzi kwa ushiriki wao katika semina ya jasiriamali.
habbari na Yasinta Peter
Wanafunzi wa
chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji Arusha wametakiwa kujishughulisha na
biashara pamoja na kuwa na tabia ya kujiwekea akiba kwa ajili ya maendeleo.
Hayo yamesemwa na Mkuu wa chuo hicho Bw.Joseph Mayagila wakati akifungua semina ya ujasiriamali ambayo ilifanyika kwa siku tatu chuoni hapo kuanzia tarehe 1 mpaka tarehe 3 Octoba mwaka huu chuoni hapo.
Bw.Mayagila ameongeza kuwa wanafunzi wengi hawana tabia ya kujiwekea akiba katika fedha ambazo wanatumiwa na wazazi wao kwa ajili ya matumizi na kuwaasa wanafunzi hao wawe wanajiwekea akiba kwa maendeleo yao.
Katika semina hiyo walimu wa chuo hicho waliyoa mada mbalimbali zikiwemo za mpango wa biashara,miongozo ya mjasiriamali,namna ya kutathmini biashara pamoja na nyingine nyingi ambapo wanafunzi wote wa chuo hicho walishiriki.
Pia ili kuongeza vionjo katika semina hiyo kulikuwepo na burudani mbalimbali ambapo wanafunzi walipewa fursa ya kuonyesha vipaji vyao mbele wanafunzi wenzao na burudani hizo ni pamoja na kuimba pamoja na vichekesho.
Nao wanafunzi wa chuo hicho wamesema kuwa wamefurahishwa na uwepo wa semina hiyo kwa sababu imewafunza mambo mbalimbali juu ya ujasiriamali ambayo hawakuwa wakiyafahamu.
Mmoja wa
wanafunzi hao Bi.Edna Lucas alikuwa na haya ya kusema,
‘’Semina ni
nzuri na nimeweza kujifunza mambo mengi ambayo sikuwa nayajua na kwa kupitia
semina hii nimehamasika kufanya biashara’’.
Akizungumza ili kuhitimisha semina hiyo makamu mkuu wa chuo Bw.Elifuraha Samboto amewataka wanafunzi kuwaheshimu walimu na vilevile wawe na tabia ya kjisomea.
Bw.Samboto alimaliza kwabkuwashukuru walimu na wanafunzi kwa ushiriki wao katika semina ya jasiriamali.