NICE MEDIA WORKS

KWA WAIMBAJI WA INJILI

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Wednesday, October 22, 2014

CHADEMA KUIPELEKA MAHAKAMANI KATIBA ILIYOPENDEKEZWA ISIPIGIWE KURA NA WANANCHI


Chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema kimesema kinakamilisha ushahidi ili kwenda mahakamani kupinga katiba inayopendekezwa kupelekwa katika hatua ya kupigiwa kura ya maoni kwa madai kuwa katiba hiyo imekosa uhalali kutokana na kukosa theluthi mbili kutoka upande wa Zanzibar.
Makamu mwenyekiti wa Chadema Tanzania Bara Profesa Abdalah Safari ametoa tamkoa hilo wakati akihutubia umati wa wakazi wa mji wa Iringa na vitongoji vyake kwenye uwanja wa Mlandege ambapo amebainisha kuwa zoezi la kupitisha rasimu ya katiba inayopendekezwa ndani ya Bunge maalumu la katiba liligubikwa na mbinu chafu za uchakachuaji wa kura hasa za wajumbe wa Zanzibar.
 
Kwa upande wake katibu mkuu wa chama hicho Dokta Wilbrod Slaa amesema chama cha mapinduzi kimeanza kuhujumu mchakato wa uandikishaji wa wananchi kwenye Daftarai la Makazi kwa kuendesha zoezi hilo kwa siri huku kikitumia mabalozi wa nyumba kumi wa chama hicho kinyume na utaratibu wa kawaida ambapo kazi hiyo inapaswa kufanywa na watendaji wa vijiji kata na mitaa.
 
Aidha katibu mkuu huyo wa Chadema amewataka wananchi kutodanganyika na vipengele vya haki za makundi mbalimbali zilizowekwa kwenye katiba hiyo pendekezwa akieleza kuwa zimewekwa kama chambo kwani haki hizo zimeondolewa na kifungu cha 21 kinachoeleza kuwa haki hizo hazitadaiwa mahakamani

Tuesday, October 7, 2014

UJASIRIAMALI NI MKOMBOZI WA MAISHA..ARUSHA

Mkurugenzi wa mafunzo katika chuo cha uandishi wa habari na utangazaji arusha bwana Joseph Mayagila Akifungua semina ya ujasiriamali iliyofanyika chuoni hapo hivi karibuni...
habbari na Yasinta Peter
Wanafunzi wa chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji Arusha wametakiwa kujishughulisha na biashara pamoja na kuwa na tabia ya kujiwekea akiba kwa ajili ya maendeleo.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa chuo hicho Bw.Joseph Mayagila  wakati akifungua semina ya ujasiriamali ambayo ilifanyika kwa siku tatu chuoni hapo kuanzia tarehe 1 mpaka tarehe 3 Octoba mwaka huu chuoni hapo.

Bw.Mayagila ameongeza kuwa wanafunzi wengi hawana tabia ya kujiwekea akiba katika fedha ambazo wanatumiwa na wazazi wao kwa ajili ya matumizi na kuwaasa wanafunzi hao wawe wanajiwekea akiba kwa maendeleo yao.

Katika semina hiyo walimu wa chuo hicho waliyoa mada mbalimbali zikiwemo za mpango wa biashara,miongozo ya mjasiriamali,namna ya kutathmini biashara pamoja na nyingine nyingi ambapo wanafunzi wote wa chuo hicho walishiriki.

Pia ili kuongeza vionjo katika semina hiyo kulikuwepo na  burudani mbalimbali ambapo wanafunzi walipewa fursa ya kuonyesha vipaji vyao mbele wanafunzi wenzao na burudani hizo ni pamoja na kuimba pamoja na vichekesho.

Nao wanafunzi wa chuo hicho wamesema kuwa wamefurahishwa na uwepo wa semina hiyo kwa sababu imewafunza mambo mbalimbali juu ya ujasiriamali ambayo hawakuwa wakiyafahamu.

Mmoja wa wanafunzi hao Bi.Edna Lucas alikuwa na haya ya kusema,
‘’Semina ni nzuri na nimeweza kujifunza mambo mengi ambayo sikuwa nayajua na kwa kupitia semina hii nimehamasika kufanya biashara’’.

Akizungumza ili kuhitimisha semina hiyo makamu mkuu wa chuo Bw.Elifuraha Samboto amewataka wanafunzi  kuwaheshimu walimu na vilevile wawe na tabia ya kjisomea.

Bw.Samboto alimaliza kwabkuwashukuru walimu na wanafunzi kwa ushiriki wao katika semina ya jasiriamali.